Ayubu 8
1 Kisha Bildadi Mshuhi akajibu:
2 “Hata lini wewe utasema mambo kama haya? Maneno yako ni kama upepo mkuu.
3 Je, Mungu hupotosha hukumu? Je, Mwenyezi hupotosha kile kilicho haki?
4 Watoto wako walipomtenda dhambi, aliwapa adhabu ya dhambi yao.
5 Lakini ukimtafuta Mungu, nawe ukamsihi Mwenyezi,
6 ikiwa wewe ni safi na mnyofu, hata sasa atainuka mwenyewe kwa niaba yako, na kukurudisha katika mahali pako pa haki.
7 Ijapokuwa mwanzo wako ulikuwa mdogo, lakini mwisho wako utakuwa wa mafanikio.
8 “Ukaulize vizazi vilivyotangulia na uone baba zao walijifunza nini,
9 kwa kuwa sisi tumezaliwa jana tu na hatujui lolote, nazo siku zetu duniani ni kama kivuli tu.
10 Je, hawatakufundisha na kukueleza? Je, hawataleta maneno ya ufahamu wao?
11 Je, mafunjo yaweza kumea mahali pasipo na matope? Matete yaweza kustawi bila maji?
12 Wakati bado yanaendelea kukua kabla ya kukatwa, hunyauka haraka kuliko majani mengine.
13 Huu ndio mwisho wa watu wote wanaomsahau Mungu; vivyo hivyo matumaini ya wasiomjali Mungu huangamia.
14 Lile analolitumainia huvunjika upesi; lile analolitegemea ni utando wa buibui.
15 Huutegemea utando wake, lakini hausimami; huung’ang’ania, lakini haudumu.
16 Yeye ni kama mti ulionyeshewa vizuri wakati wa jua, ukieneza machipukizi yake bustanini;
17 huifunganisha mizizi yake kwenye lundo la mawe, na kutafuta nafasi kati ya mawe.
18 Unapong’olewa kutoka mahali pake, ndipo mahali pale huukana na kusema, ‘Mimi kamwe sikukuona.’
19 Hakika uhai wake hunyauka, na kutoka udongoni mimea mingine huota.
20 “Hakika Mungu hamkatai mtu asiye na hatia, wala kuitia nguvu mikono ya mtenda maovu.
21 Bado atakijaza kinywa chako na kicheko, na midomo yako na kelele za shangwe.
22 Adui zako watavikwa aibu, nayo mahema ya waovu hayatakuwepo tena.”
Перекрёстные ссылки
144
- 1Job 2:11
- 2Job 6:26, Job 15:2, 1Ki 19:11, Job 11:2–3, Job 18:2, Job 16:3, Exo 10:7, Job 6:9
- 3Deu 32:4, 2Ch 19:7, Gen 18:25, Job 34:10–12, Rom 3:4–6, Dan 9:14, Ezk 33:20, Job 40:8
- 4Job 1:5, Job 1:18–19, Job 5:4, Job 18:16–19, Gen 19:13–25, Gen 13:13
- 5Jas 4:7–10, Job 11:13, Heb 3:7–8, Isa 55:6–7, Mat 7:7–8, 2Ch 33:12–13, Job 5:8, Job 22:21–30
- 6Isa 51:9, Job 5:24, Isa 3:10, Psa 7:6, Pro 15:8, Psa 59:4–5, Job 16:17, Job 4:6–7
- 7Job 42:12–13, Mat 13:31–32, Pro 19:20, Zec 4:10, Pro 4:18, Zec 14:7, Mat 13:12, Deu 8:16
- 8Job 15:18, Deu 32:7, Deu 4:32, Rom 15:4, 1Co 10:11, Job 32:6–7, Isa 38:19, Psa 44:1
- 91Ch 29:15, Psa 144:4, Job 14:2, Psa 102:11, Job 7:6, Gen 47:9, Psa 90:4, Psa 39:5
- 10Pro 18:15, Mat 12:35, Pro 16:23, Job 32:7, Job 12:7–8, Heb 12:1, Deu 6:7, Psa 145:4
- 11Exo 2:3, Isa 19:5–7
- 12Jer 17:6, Mat 13:20, 1Pe 1:24, Psa 129:6–7, Jas 1:10–11
- 13Psa 9:17, Job 13:16, Job 11:20, Job 15:34, Pro 10:28, Job 20:5, Deu 8:11, Deu 8:19
- 14Isa 59:5–6
- 15Job 27:18, Mat 7:24–27, Luk 6:47–49, Psa 52:5–7, Pro 10:28, Job 18:14, Psa 49:11, Psa 112:10
- 16Psa 80:11, Psa 73:3–12, Jer 11:16, Psa 37:35–36, Job 5:3, Job 21:7–15
- 17Isa 40:24, Job 29:19, Mrk 11:20, Job 18:16, Jer 12:1–2, Isa 5:24, Jud 1:12
- 18Job 7:10, Job 7:8, Psa 37:36, Psa 37:10, Psa 92:7, Psa 73:18–19, Job 20:9
- 19Job 20:5, 1Sa 2:8, Psa 113:7, Psa 75:7, Mat 13:20–21, Mat 3:9, Ezk 17:24
- 20Job 4:7, Psa 37:37, Psa 37:24, Isa 45:1, Psa 94:14, Job 21:30, Job 9:22
- 21Psa 126:2, Gen 21:6, Psa 126:6, Psa 32:11, Luk 6:21, Isa 65:13–14, Job 5:22, Ezr 3:11–13
- 22Psa 132:18, Psa 35:26, Psa 109:29, Job 18:14, Job 8:18, Job 7:21, 1Pe 5:5