Hosea 14
1 Rudi, ee Israeli, kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wako. Dhambi zako zimekuwa anguko lako!
2 Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie Mwenyezi Mungu. Mwambieni: “Samehe dhambi zetu zote na utupokee kwa neema, ili tuweze kutoa matunda yetu kama sadaka za mafahali.
3 Ashuru hawezi kutuokoa, hatutapanda farasi wa vita. Kamwe hatutasema tena ‘miungu yetu’ kwa kile ambacho mikono yetu wenyewe imetengeneza, kwa kuwa kwako wewe yatima hupata huruma.”
4 “Nitaponya ukaidi wao na kuwapenda kwa hiari yangu, kwa kuwa hasira yangu imeondoka kwao.
5 Nitakuwa kama umande kwa Israeli; atachanua kama yungiyungi. Kama mwerezi wa Lebanoni atashusha mizizi yake chini;
6 matawi yake yatatanda. Fahari yake itakuwa kama mti wa mzeituni, harufu yake nzuri kama mwerezi wa Lebanoni.
7 Watu wataishi tena kwenye kivuli chake. Atastawi kama nafaka. Atachanua kama mzabibu, nao umaarufu wake utakuwa kama divai inayotoka Lebanoni.
8 Ee Efraimu, nina shughuli gani tena na sanamu? Nitamjibu na kumtunza. Mimi ni kama msunobari wenye majani mabichi; kuzaa kwako matunda kunatoka kwangu.”
9 Ni nani mwenye hekima? Atayatambua mambo haya. Ni nani mwenye ufahamu? Huyu atayaelewa. Njia za Mwenyezi Mungu ni adili; wenye haki huenda katika njia hizo, lakini waasi watajikwaa ndani yake.
Перекрёстные ссылки
72
- 1Hos 6:1, Jol 2:12–13, Hos 12:6, 2Ch 30:6–9, Zec 1:3–4, Jer 4:1, Act 26:18–20, Isa 55:6–7
- 2Psa 51:2–10, Heb 13:15, Job 34:31–32, Job 7:21, Mic 7:18–19, 1Jn 3:5, Psa 69:30–31, 2Sa 12:13
- 3Psa 10:14, Psa 68:5, Isa 31:1, Psa 33:17, Hos 14:8, Hos 5:13, Hos 2:17, Isa 30:16
- 4Isa 57:18, Jer 3:22, Isa 12:1, Eph 2:4–9, Zep 3:17, Hos 6:1, Jer 14:7, 2Co 5:19–21
- 5Isa 35:2, Isa 27:6, Eph 3:17, Mat 6:28, Isa 44:3, Isa 26:19, Job 29:19, Mic 5:7
- 6Psa 52:8, Psa 128:3, Php 4:18, Mat 13:31, Jhn 15:1, Rom 11:16–24, Jer 11:16, Dan 4:10–15
- 7Psa 91:1, Jhn 11:25, Hos 14:5, Zec 8:12, Isa 32:1–2, Ezk 17:23, Sng 6:11, Psa 138:7
- 8Job 34:32, Jas 1:17, Isa 55:13, Luk 15:20, Php 2:13, Isa 41:19, 1Pe 4:3–4, Php 1:11
- 9Pro 10:29, Psa 107:43, Jhn 8:47, Dan 12:10, Pro 1:5–6, Psa 19:7–8, Deu 32:4, Zep 3:5