Habakuki 1
1 Neno la unabii alilopokea nabii Habakuki.
2 Ee Mwenyezi Mungu, hata lini nitakuomba msaada, lakini wewe husikilizi? Au kukulilia, “Udhalimu!” lakini hutaki kuokoa?
3 Kwa nini unanifanya nitazame dhuluma? Kwa nini unavumilia makosa? Uharibifu na udhalimu viko mbele yangu; kuna mabishano na mapambano kwa wingi.
4 Kwa hiyo sheria imepotoshwa, nayo haki haipo kabisa. Waovu wanawazunguka wenye haki, kwa hiyo haki imepotoshwa.
5 “Yatazame mataifa, uangalie na ushangae kabisa. Kwa sababu katika siku zako nitafanya kitu ambacho hungeamini, hata kama ungeambiwa.
6 Tazama! Nitawainua Wakaldayo, watu wakatili na wenye haraka, ambao hupita dunia yote ili kuteka makazi yasiyo yao.
7 Ni watu wanoogopwa na wanaotisha; wenyewe ndio sheria yao, na huinua heshima yao wenyewe.
8 Farasi wao ni wepesi kuliko chui, na wakali kuliko mbwa-mwitu wakati wa machweo. Askari wapanda farasi wao huenda mbio; waendesha farasi wao wanatoka mbali. Wanaruka kasi kama tai ili kurarua mawindo;
9 wote wanakuja tayari kutenda udhalimu. Makundi yao wanasonga mbele kama upepo wa jangwani, na kukusanya wafungwa kama mchanga.
10 Wanawabeza wafalme, na kuwadhihaki watawala. Wanaicheka miji yote yenye ngome; wanalundika udongo na kuiteka hiyo miji.
11 Kisha wanapita kasi kama upepo na kusonga mbele: watu wenye hatia, ambao nguvu zao ndio mungu wao.”
12 Ee Mwenyezi Mungu, je, wewe sio wa tangu milele? Mungu wangu, Uliye Mtakatifu wangu, hatutakufa. Ee Mwenyezi Mungu, umewachagua wao ili watekeleze hukumu; Ee Mwamba, umewaamuru watuadhibu.
13 Macho yako ni safi mno hata yasiweze kuutazama uovu, wala huwezi kuvumilia makosa. Kwa nini basi unawavumilia wadanganyifu? Kwa nini unakuwa kimya wakati waovu wanawameza wale wenye haki kuliko wao wenyewe?
14 Umewafanya watu kama samaki baharini, kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.
15 Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana, anawakamata katika wavu wake, anawakusanya katika juya lake; kwa hiyo anashangilia na anafurahi.
16 Kwa hiyo anatoa sadaka kwa wavu wake, na kuchoma uvumba kwa juya lake, kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe, na anafurahia chakula kizuri.
17 Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake, akiangamiza mataifa bila huruma?
Referencias cruzadas
115
- 1Nam 1:1, Isa 22:1
- 2Psa 22:1–2, Psa 13:1–2, Lam 3:8, Jer 14:9, Rev 6:10, Psa 94:3, Psa 74:9–10
- 3Psa 55:9–11, Mic 7:1–4, Jer 9:2–6, Ecc 5:8, Jer 20:8, Ezk 2:6, Psa 12:1–2, Mat 10:16
- 4Psa 94:20–21, Psa 119:126, Job 21:7, Isa 1:21–23, Jer 12:1, Ezk 9:9, Isa 59:13–15, Isa 5:20
- 5Act 13:40–41, Isa 29:14, Lam 4:12, Jer 5:12–13, Isa 29:9, Jer 9:25–26, Jer 25:14–29, Jer 18:18
- 62Ki 24:2, 2Ch 36:6, Jer 5:15, 2Ch 36:17, Jer 4:6, Deu 28:49–52, Isa 23:13, Jer 25:9
- 7Jer 39:5–9, Deu 5:19, Jer 52:25–27, Jer 52:9–11, Deu 5:27, Isa 18:7
- 8Jer 4:13, Zep 3:3, Hos 8:1, Deu 28:49, Ezk 17:3, Jer 5:6, Isa 5:26–28, Ezk 17:12
- 9Jer 25:9, Isa 27:8, Jer 4:11, Psa 139:18, Hab 2:5–13, Hos 13:15, Ezk 17:10, Hab 1:6
- 102Ch 36:6, 2Ch 36:10, Isa 14:16, Jer 32:24, Jer 52:4–7, Jer 33:4, 2Ki 25:6–7, 2Ki 24:12
- 11Dan 5:20, Dan 4:30–34, Jer 4:11–12, Dan 5:3–4
- 12Deu 32:4, Psa 90:2, Deu 33:27, Jer 46:28, Jer 30:11, Psa 93:2, Amo 9:8–9, Ezk 37:11–14
- 13Psa 5:4–5, Psa 34:15–16, Jer 12:1–2, Hab 1:3–4, Pro 31:8–9, Psa 50:3, Psa 10:15, 2Sa 4:11
- 15Amo 4:2, Jer 16:16, Psa 10:9, Jhn 21:6–11, Ezk 26:2, Isa 19:8, Rev 11:10, Ezk 25:6
- 16Dan 4:30, Ezk 28:3, Deu 8:17, Hab 1:11, Ezk 29:3, Isa 37:24, Dan 5:23, Isa 10:13–15
- 17Hab 1:9–10, Jer 25:9–26, Hab 2:17, Hab 2:5–8, Jer 52:1–34, Isa 14:16–17, Isa 14:6, Jer 46:1–28
Temas en este capítulo
26
Afflictions and Adversities, Anthropomorphisms, Babylon, Chaldea, Covetousness, Eye, Faith, Fish, God, Habakkuk, Happiness, Idolatry, Israel, Prophecies Concerning, Justice, Leopard, Minister, Christian, Persecution, Prayer, Prophecy, Punishment, Quotations and Allusions, Rulers, Sin, Strife, Wicked (People), Zeal, Religious