Ezra 9
1 Baada ya mambo haya kutendeka, viongozi walinijia na kusema, “Watu wa Israeli, wakiwemo makuhani na Walawi, hawakujitenga na majirani zao katika kufanya machukizo, kama yale ya Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wayebusi, Waamoni, Wamoabu, Wamisri na Waamori.
2 Wamewaoa baadhi ya binti zao kuwa wake zao na wake za wana wao, nao wamechanganya taifa takatifu na watu waliowazunguka. Nao viongozi na maafisa wamekuwa mstari wa mbele katika njia hii potovu.”
3 Niliposikia jambo hili nilirarua koti langu na joho langu, nikazing’oa nywele za kichwa changu na ndevu zangu na kuketi nikishangaa.
4 Kisha kila mmoja aliyetetemeshwa na maneno ya Mungu wa Israeli alikusanyika kunizunguka kwa sababu ya upotovu huu wa hao watu waliorudi kutoka utumwani. Nami niliketi pale nikishangaa hadi wakati wa dhabihu ya jioni.
5 Ndipo wakati wa kutoa dhabihu ya jioni nikainuka kutoka kujidhili kwangu nikiwa na koti na joho langu lililoraruka, nikapiga magoti mikono yangu ikiwa imeinuliwa kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wangu.
6 Nami nikaomba: “Ee Mungu wangu, natahayari na kuona aibu kukuinulia uso wangu Mungu wangu, kwa sababu dhambi zetu zimejikusanya hata kupita juu ya vichwa vyetu na hatia yetu imefika mbinguni.
7 Tokea siku za babu zetu hadi sasa, hatia yetu imekuwa kubwa. Kwa sababu ya dhambi zetu, sisi na wafalme wetu na makuhani wetu tumekabiliwa na vita, utumwa, kutekwa na kudhiliwa katika mikono ya wafalme wa kigeni, kama ilivyo leo.
8 “Lakini sasa, kwa muda mfupi, Mwenyezi Mungu, Mungu wetu, amekuwa na neema kwa kutuachia mabaki na kutupatia mahali imara katika mahali pake patakatifu, hivyo Mungu wetu anatupatia mwanga machoni petu na unafuu katika utumwa wetu.
9 Ingawa tu watumwa, Mungu wetu hajatuacha katika kufungwa kwetu. Ametuonesha huruma mbele ya wafalme wa Uajemi: Ametujalia maisha mapya kwa kujenga upya nyumba ya Mungu wetu na kukarabati magofu yake, naye ametupatia ukuta wa ulinzi katika Yuda na Yerusalemu.
10 “Lakini sasa, Ee Mungu wetu, tunaweza kusema nini baada ya hili? Kwa maana tumedharau maagizo
11 uliyoyatoa kupitia watumishi wako manabii uliposema: ‘Nchi mnayoiingia kuimiliki ni nchi iliyochafuliwa na uovu wa watu wake. Kwa matendo yao ya machukizo wameijaza nchi kwa unajisi wao kutoka mwisho mmoja hadi mwingine.
12 Kwa hiyo, msiwaoze binti zenu kwa wana wao wala binti zao kwa wana wenu. Msitafute mkataba wa urafiki nao kwa wakati wowote. Ndipo mtakapofanikiwa na kula mema ya nchi na kuwaachia watoto wenu nchi hiyo kama urithi wao wa milele.’
13 “Yale yaliyotupata ni matokeo ya matendo yetu mabaya, pia hatia yetu kubwa. Hata hivyo, wewe Mungu wetu, umetuadhibu kidogo kuliko dhambi zetu zilivyostahili na umetupatia mabaki kama haya.
14 Je, tutavunja maagizo yako tena na kuoana na watu ambao hufanya mambo ya machukizo? Je, hutakuwa na hasira ya kutosha juu yetu na kutuangamiza, bila kutuachia mabaki wala atakayenusurika?
15 Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki! Siku ya leo tumeachwa kama mabaki. Tupo hapa mbele zako na hatia yetu, ingawa katika hali hii hakuna hata mmoja wetu anayeweza kusimama mbele zako.”
Referencias cruzadas
117
- 1Lev 18:24–30, Neh 9:2, Ezr 10:10–11, Rom 2:17–25, Exo 33:16, Deu 12:30–31, 2Ch 33:2, Gen 15:16
- 2Neh 13:23–24, Ezr 10:2, Ezr 10:18–44, Exo 34:16, Deu 7:6, Deu 7:1–4, Exo 22:31, Deu 14:2
- 3Neh 1:4, Jos 7:6, Job 2:12–13, Ezk 7:18, Isa 15:2, Dan 4:19, Lev 21:5, Mic 1:16
- 4Ezr 10:3, Isa 66:2, Exo 29:39, Psa 119:136, 2Ch 34:27, Ezk 9:4, Act 3:1, Dan 9:21
- 51Ki 8:38, 1Ki 8:54, 1Ki 8:22, Exo 9:29, Exo 9:33, Psa 95:6, 2Ch 6:13, Psa 141:2
- 6Rev 18:5, Psa 38:4, 2Ch 28:9, Job 42:6, Ezr 9:15, Luk 15:21, Jer 3:24–25, Dan 9:7–8
- 72Ch 29:6, Dan 9:5–8, Neh 9:30, Act 7:51–52, Jer 44:22, 2Ch 36:16–19, Lam 5:7, Dan 9:11–14
- 8Psa 13:3, Rom 11:5–6, Hos 6:2, Hab 3:2, Ezk 37:11–14, Isa 57:15, Psa 85:6, Zec 10:4
- 9Psa 136:23–24, Ezr 7:6, Hag 1:9, Psa 106:45–46, Zec 2:5, Zec 4:6–10, Ezr 6:14–15, Dan 9:25
- 10Jos 7:8, Dan 9:4–16, Gen 44:16, Rom 3:19, Lam 3:22
- 11Lev 18:24–30, Ezr 6:21, Ezr 9:1, Deu 18:12, Ezk 36:25–27, 2Co 7:1, Deu 12:31, 2Ch 33:2
- 12Deu 7:3, Deu 23:6, Jos 23:12–13, Pro 13:22, Exo 34:15–16, 2Jn 1:10–11, Pro 20:7, Psa 112:1–2
- 13Psa 103:10, Lam 3:39–40, Lam 3:22, Job 11:6, Ezr 9:6–8, Psa 106:45–46, Neh 9:32, Ezk 24:13–14
- 14Deu 9:8, Ezr 9:2, Deu 9:14, Rom 6:1, Jhn 5:14, Num 16:45, Jdg 2:2, Num 16:21
- 15Psa 130:3, Jhn 8:24, Rom 3:19, Jhn 8:21, Rom 10:3, Neh 9:33–34, Zec 3:3–4, Isa 64:6–7
Temas en este capítulo
38
Afflictions and Adversities, Ammonites, Amorites, Backsliders, Beard, Blushing, Bondage, Canaanites, Captivity, Church, Company, Dress, Ezra, Fellowship, God, Government, Hittites, Humility, Influence, Intercession, Israel, Prophecies Concerning, Jebusites, Levites, Mantle, Marriage, Minister, Christian, Moabites, Mourning, Nail, Nation, Perizzites, Prayer, Priest, Rending, Repentance, Sin, Wicked (People), Zeal, Religious