1 Wakorintho 12
1 Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au nyingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
3 Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho Mtakatifu wa Mungu anayeweza kusema, “Isa na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Isa ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho wa Mungu.
4 Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
5 Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana Isa ni yule yule.
6 Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho wa Mungu kwa faida ya wote.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
9 Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
10 Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii, kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine kunena aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
11 Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
12 Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi; navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Al-Masihi.
13 Kwa maana katika Roho mmoja wa Mungu wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
14 Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
17 Kama mwili wote ungakuwa jicho tu, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungekuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
18 Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
22 Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
23 Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
24 wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
25 ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho; kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
27 Sasa ninyi ni mwili wa Al-Masihi na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
28 Mungu ameweka katika jumuiya ya waumini kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, na aina mbalimbali za lugha.
29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
30 Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
31 Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonesha njia iliyo bora zaidi.
Cross-references
171
- 11Co 12:4–11, 1Co 14:37, 1Co 14:1–18, Eph 4:11
- 21Pe 4:3, 1Th 1:9, Psa 115:5, Gal 4:8, Eph 2:11–12, 1Co 6:11, Jer 10:5, Hab 2:18–19
- 31Jn 4:2–3, Rom 10:9, Mat 16:16–17, 2Co 3:5, Jhn 13:13, 1Co 8:6, Jhn 15:26, Mat 22:43
- 41Pe 4:10, 1Co 12:28, Rom 12:4–6, 1Co 12:8–11, Heb 2:4, Eph 4:4–6, Eph 4:11
- 5Eph 4:11–12, Rom 12:6–8, Rom 14:8–9, 1Co 8:6, Mat 23:10, 1Co 12:28–29, Act 10:36, Php 2:11
- 61Co 3:7, Jhn 5:17, 1Co 12:11, Eph 4:6, Col 3:11, Heb 13:21, Php 2:13, Col 1:29
- 71Pe 4:10–11, Rom 12:6–8, 1Co 14:19, 1Co 14:12, 1Co 14:17, Eph 4:7–12, 1Co 14:22–26, 1Co 14:5
- 8Pro 2:6, 1Co 2:6–10, Eph 1:17–18, Psa 143:10, 2Co 8:7, 1Co 1:5, Neh 9:20, Isa 11:2–3
- 9Jas 5:14–15, 2Co 4:13, Eph 2:8, Heb 11:33, Mat 17:19–20, 1Co 13:2, 1Co 12:28, Mat 21:21
- 101Co 14:39, 1Jn 4:1, Mrk 16:17, 1Co 12:28–30, 1Co 14:31–32, Jol 2:28, Mrk 16:20, 1Co 14:26–29
- 11Heb 2:4, 1Co 12:4, 2Co 10:13, 1Co 12:6, Eph 4:7, 1Co 7:7, Mat 11:26, 1Co 7:17
- 12Rom 12:4–5, Col 3:15, 1Co 12:27, Eph 4:15–16, Col 2:19, Eph 5:30, 1Co 10:17, Eph 4:4
- 13Eph 4:5, Col 3:11, Gal 3:28, Jhn 7:37–39, 1Pe 3:21, Rom 6:3–6, Act 1:5, Rom 3:29
- 141Co 12:27–28, 1Co 12:12, 1Co 12:19, Eph 4:25
- 15Jdg 9:8–15, 2Ki 14:9
- 16Rom 12:3, Rom 12:10, Php 2:3, 1Co 12:22
- 17Psa 139:13–16, Pro 20:12, 1Co 12:21, Psa 94:9, 1Co 12:29
- 181Co 12:28, Rom 12:3, 1Co 12:11, Luk 12:32, 1Co 3:5, Psa 135:6, 1Co 12:24, Luk 10:21
- 201Co 12:14, 1Co 12:12
- 21Neh 4:16–21, Ezr 10:1–5, Job 29:11
- 22Pro 14:28, Ecc 9:14–15, Ecc 4:9–12, 2Co 1:11, Ecc 5:9
- 23Gen 3:21
- 24Gen 3:11, Gen 2:25
- 252Co 13:11, 1Co 1:10–12, Jhn 17:21–26, 2Co 8:16, 2Co 7:12, 1Co 3:3
- 26Rom 12:15, Gal 6:2, Heb 13:3, 1Pe 3:8
- 27Eph 4:12, Eph 5:30, Col 1:24, Rom 12:5, 1Co 12:12, 1Co 12:14–20, Eph 5:23, Eph 1:23
- 28Eph 4:11–13, Rom 12:6–8, 1Co 12:18, 1Co 12:7–11, 1Ti 5:17, Eph 2:20, Eph 3:5, Heb 13:24
- 291Co 12:4–11, 1Co 12:14–20
- 301Co 12:10
- 311Co 13:1–14:1, 1Co 14:39, Php 3:8, Mat 5:6, Luk 10:42, 1Co 8:1, Heb 11:4
Topics in this chapter
32
Baptism, Blasphemy, Blessing, Charism, Church, Communion, Confession, Faith, Fellowship, Gentiles, Gifts From God, God, Greece, Holiness, Holy Spirit, Idolatry, Instruction, Interpreter, Knowledge, Language, Miracles, Prophets, Regeneration, Righteous, Righteousness, Servant, Symbols and Similitudes, Testimony, Tongue, Tongues (the Gift), Trinity, Wisdom