Wimbo Ulio Bora 1
1 Wimbo ulio bora wa Sulemani.
2 Unibusu kwa busu la kinywa chako, kwa maana upendo wako unafurahisha kuliko divai.
3 Manukato yako yananukia vizuri, jina lako ni kama manukato yaliyomiminwa. Ndiyo sababu wanawali wanakupenda!
4 Nichukue twende nawe, na tufanye haraka! Mfalme na anilete ndani ya vyumba vyake. Rafiki Tunakushangilia na kukufurahia, tutasifu upendo wako kuliko divai. Mpendwa Tazama jinsi ilivyo bora wakupende!
5 Mimi ni mweusi, lakini napendeza, enyi binti za Yerusalemu, mweusi kama mahema ya Kedari, kama mapazia ya hema la Sulemani.
6 Usinikazie macho kwa sababu mimi ni mweusi, kwa sababu nimefanywa mweusi na jua. Wana wa mama yangu walinikasirikia na kunifanya niwe mtunza mashamba ya mizabibu. Shamba langu mwenyewe la mizabibu nimeliacha.
7 Niambie, wewe ninayekupenda, unalisha wapi kundi lako la kondoo na ni wapi unapowapumzisha kondoo wako adhuhuri. Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefunikwa shela karibu na makundi ya rafiki zako?
8 Kama hujui, ewe mwanamke mzuri kuliko wote, fuata nyayo za kondoo, na kulisha wana-mbuzi wako karibu na mahema ya wachungaji.
9 Mpendwa wangu, ninakufananisha na farasi jike aliyefungwa katika mojawapo ya magari ya vita ya Farao.
10 Mashavu yako yanapendeza yakiwa na vipuli, shingo yako ikiwa na mikufu ya vito.
11 Tutakufanyia vipuli vya dhahabu, vyenye kupambwa kwa fedha.
12 Mfalme alipokuwa mezani pake, manukato yangu yalisambaza harufu yake nzuri.
13 Mpenzi wangu kwangu mimi ni kifuko cha manemane kati ya matiti yangu.
14 Mpenzi wangu kwangu mimi ni kama kishada cha maua ya mhina kutoka mashamba ya mizabibu ya En-Gedi.
15 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpendwa wangu! Tazama jinsi ulivyo mzuri! Macho yako ni kama ya hua.
16 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Ee, tazama jinsi unavyopendeza! Na kitanda chetu ni cha majani mazuri.
17 Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, na mapao yetu ni miberoshi.
Cross-references
122
- 2Sng 4:10, Psa 36:7, Sng 1:4, Isa 55:1–2, Psa 63:3–5, Mat 26:26, Sng 7:9, Luk 15:20
- 3Ecc 7:1, Exo 30:23–28, Jhn 12:3, Sng 4:10, Php 2:9–10, Psa 45:7–8, Rev 14:4, Psa 45:14
- 4Jhn 6:44, Hos 11:4, Psa 45:14–15, Jhn 12:32, Jer 31:3, Heb 12:1, Isa 25:8, Sng 3:4
- 5Luk 15:22, Sng 2:14, Sng 2:7, Sng 5:16, Psa 120:5, Sng 5:8, 2Co 5:21, Rom 13:14
- 6Sng 8:11–12, Luk 12:51–53, Jer 12:6, Job 30:30, Psa 69:8, Mrk 4:6, Mat 10:22, Lam 4:8
- 7Sng 3:1–4, Isa 13:20, Psa 23:1–2, Gen 37:16, Psa 28:1, Isa 40:11, 1Pe 1:8, Sng 8:13
- 8Sng 6:1, Sng 5:9, Jas 2:21, Jas 5:10, Heb 11:4–40, Psa 16:3, Jer 6:16, Jhn 21:15
- 9Sng 2:10, Sng 2:13, Jhn 15:14–15, Sng 1:15, Isa 31:1, Sng 4:7, Sng 2:2, Sng 5:2
- 10Ezk 16:11–13, 1Pe 3:4, Sng 5:13, Gen 24:47, Pro 1:9, 2Pe 1:3–4, Gen 41:42, Sng 4:9
- 11Psa 149:4, Php 3:21, Gen 1:26, Sng 8:9, Eph 5:25–27
- 12Jhn 12:3, Rev 3:20, Mrk 14:3, Psa 45:1, Luk 24:30–32, Php 4:18, Sng 7:5, Sng 4:13–16
- 13Jhn 19:39, Psa 45:8, Eph 3:17, Sng 5:1, Gen 43:11, Sng 8:3–4, Sng 4:14, Sng 2:7
- 14Sng 2:3, 1Sa 23:29–24:1, Jos 15:62, Sng 1:13, Sng 4:13–14
- 15Sng 4:1, Sng 5:12, Sng 4:7, Eph 1:17–18, 2Co 11:2–3, Sng 6:4, Sng 7:6, Sng 1:8
- 16Sng 2:3, Psa 45:2, Zec 9:17, Psa 110:3, Sng 3:7, Php 3:8–9, Rev 5:11–13, Sng 5:10–16
- 17Heb 11:10, Psa 92:12, 2Ch 2:8–9, 1Ti 3:15–16, Ezk 41:16, 1Ki 6:9, Sng 8:9, Ezk 42:3