Isaya 15
1 Neno la unabii kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!
2 Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, hadi mahali pake pa juu pa kuabudia ili walie, Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. Kila kichwa kimenyolewa na kila ndevu limeondolewa.
3 Wamevaa magunia barabarani; juu ya mapaa na kwenye viwanja wote wanaomboleza, wakilala kifudifudi na kulia.
4 Heshboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikika hadi Yahazi. Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, nayo mioyo yao imezimia.
5 Moyo wangu unamlilia Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Soari, hadi Eglath-Shelishiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, wanaenda huku wanalia; barabarani iendayo Horonaimu wanaombolezea maangamizi yao.
6 Maji ya Nimrimu yamekauka na majani yamenyauka; mimea imekauka wala hakuna kitu chochote kibichi kilichobaki.
7 Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
8 Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
9 Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: simba juu ya wakimbizi wa Moabu na juu ya wale wanaobaki katika nchi.
Cross-references
67
- 1Amo 2:1–3, Jer 48:1–47, Isa 11:14, Ezk 25:8–11, Num 21:28, Isa 16:7, Isa 14:28, 1Th 5:1–3
- 2Lev 21:5, Jer 48:1, Isa 3:24, Deu 34:1, Jer 48:18, Num 21:30, Ezk 7:18, Jos 13:16–17
- 3Jon 3:6–8, Isa 15:2, Deu 22:8, Isa 22:4, 2Ki 6:30, 2Sa 3:31, Isa 22:1, Mat 11:21
- 4Jer 48:34, Jos 13:18, Deu 2:32, Jon 4:3, Jdg 11:20, Jer 20:18, Job 3:20–22, Num 32:3–4
- 5Jer 48:5, Jer 4:20, Luk 19:41–44, Jer 48:31–36, 2Sa 15:30, Gen 13:10, Isa 16:14, Jer 8:18–19
- 6Isa 19:5–7, Jol 1:10–12, Num 32:36, Rev 8:7, Jos 13:27, Hab 3:17–18, Num 32:3, Isa 16:9–10
- 7Jer 48:36, Isa 30:6, Psa 137:1–2, Isa 10:6, Nam 2:12–13, Isa 5:29, Isa 10:14
- 8Ezk 47:10, Isa 15:2–5, Jer 48:31–34, Jer 48:20–24
- 92Ki 17:25, Jer 48:43–45, Lev 26:24, Amo 5:19, Lev 26:28, Jer 50:17, Jer 15:3, Lev 26:18