1 Timotheo 4
1 Roho wa Mungu asema waziwazi kwamba katika siku za mwisho baadhi ya watu wataiacha imani na kufuata roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.
2 Mafundisho kama hayo huja kupitia kwa waongo ambao ni wanafiki, hali dhamiri zao zikiungua kwa kuchomwa moto.
3 Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.
4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani,
5 kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
6 Ukiwakumbusha ndugu mambo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Al-Masihi Isa, uliyelelewa katika kweli ya imani na yale mafundisho mazuri uliyoyafuata.
7 Usijishughulishe kamwe na hadithi za kipagani na masimulizi ya uongo ya wanawake wazee; badala yake, jizoeze kuwa mtauwa.
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yana faida kwa sehemu, lakini utauwa una faida katika mambo yote, yaani unayo ahadi ya uzima wa sasa na ya ule ujao.
9 Hili ni neno la kuaminiwa tena lastahili kukubaliwa kabisa.
10 Nasi kwa ajili ya hili tunajitaabisha na kujitahidi, kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
11 Mambo haya yaagize na kuyafundisha.
12 Mtu yeyote asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe kielelezo kizuri kwa waumini katika usemi, mwenendo, upendo, imani na usafi.
13 Fanya bidii kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri na kufundisha, hadi nitakapokuja.
14 Usiache kutumia kipawa kilicho ndani yako, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee walikuwekea mikono.
15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.
16 Jilinde sana nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika hayo, kwa maana kwa kufanya hivyo, utajiokoa wewe mwenyewe pamoja na wale wanaokusikia.
Cross-references
117
- 12Ti 3:1–9, 2Pe 2:1, 2Co 11:13–15, Jud 1:18, 2Th 2:3–12, 2Pe 3:3, Jud 1:4, 2Co 11:3
- 2Eph 4:19, Rom 16:18, Act 20:30, 2Pe 2:1–3, Rev 16:14, Rom 1:28, 2Ti 3:5, Mat 24:24
- 31Ti 4:4, Heb 13:4, Rom 14:6, Col 2:16, 1Co 8:8, Gen 9:3, 1Co 10:30–31, 1Co 7:28
- 4Rom 14:20, 1Co 10:25, Rom 14:14, 1Co 10:23, Act 21:25, Act 11:7–9, 1Ti 4:3, Act 15:20–21
- 51Ti 4:3, Luk 4:4, 1Co 7:14, Tit 1:15, Luk 11:41, Gen 1:31, Gen 1:25
- 6Tit 2:7–10, Col 3:16, Col 4:7, Tit 2:1, 2Ti 3:14–17, Mat 13:52, 2Pe 3:1–2, 2Ti 2:14–15
- 72Ti 2:16, Tit 2:12, 1Ti 1:4, 2Pe 1:5–8, Tit 3:9, Heb 5:14, 2Ti 2:23, 1Ti 6:11
- 8Mat 6:33, 1Ti 6:6, Psa 37:3–4, Pro 22:4, Pro 19:23, Col 2:21–23, Psa 37:11, Psa 145:19
- 91Ti 1:15
- 101Ti 2:4, 1Jn 2:2, Jhn 1:29, 1Ti 2:6, 1Jn 4:14, Rom 15:12–13, Jhn 4:42, Jhn 3:15–17
- 111Ti 6:2, 2Ti 4:2, 1Ti 5:7, Tit 2:15, Tit 3:8
- 12Tit 2:7, 2Ti 2:22, 2Ti 2:15, 1Pe 5:3, 2Pe 1:5–8, 1Co 11:1, 1Th 1:6, 2Ti 2:7
- 13Act 6:4, 2Ti 4:2, Tit 2:15, 1Ti 4:16, Act 17:11, 2Ti 2:15–17, 1Ti 4:6, Jos 1:8
- 142Ti 1:6, 1Pe 4:9–11, 1Ti 1:18, Act 6:6, 1Ti 5:22, 1Th 5:19, Act 13:3, Mat 25:14–30
- 15Mat 5:16, Psa 143:5, Php 2:15–16, Psa 104:34, Psa 119:48, Act 6:4, 1Ti 4:6, Jos 1:8
- 16Tit 1:9, Tit 2:7, 2Jn 1:8–9, 1Co 3:10–11, Ezk 33:7–9, Act 20:26–28, Isa 55:11, 2Ti 4:2
Topics in this chapter
47
Animals, Apostasy, Asceticism, Celibacy, Charitableness, Children, Church, Commandments, Conscience, Continence, Demons, Doctrines, Elder, Example, Fable, Faith, Falsehood, Food, Gifts From God, God, Gospel, Hand, Holiness, Holy Spirit, Hypocrisy, Immortality, Iron, Life, Love, Marriage, Meditation, Minister, Christian, Miracles, Prayer, Righteous, Salvation, Sarcasm, Thankfulness, Timothy, Tradition, Truth, Vanity, Watchfulness, Word of God, Worship, Young Men, Zeal, Religious