Ezekieli 48
1 “Haya ndiyo majina ya makabila na sehemu zao: “Kwenye mpaka wa kaskazini, Dani atakuwa na sehemu moja; mpaka huo utafuata barabara ya Hethloni hadi Lebo-Hamathi; Hasar-Enani hata mpaka wa kaskazini wa Dameski karibu na Hamathi utakuwa sehemu ya huo mpaka wake kuanzia upande wa mashariki hadi upande wa magharibi.
2 Asheri atakuwa na sehemu moja; itapakana na nchi ya Dani kuanzia mashariki hadi upande wa magharibi.
3 Naftali atakuwa na sehemu moja; itapakana na nchi ya Asheri kuanzia mashariki hadi magharibi.
4 Manase atakuwa na sehemu moja; itapakana na nchi ya Naftali kuanzia mashariki hadi magharibi.
5 Efraimu atakuwa na sehemu moja; itapakana na nchi ya Manase kuanzia mashariki hadi magharibi.
6 Reubeni atakuwa na sehemu moja; itapakana na nchi ya Efraimu kuanzia mashariki hadi magharibi.
7 Yuda atakuwa na sehemu moja; itapakana na nchi ya Reubeni kuanzia mashariki hadi magharibi.
8 “Kupakana na nchi ya Yuda kuanzia mashariki mpaka magharibi itakuwa ndiyo sehemu utakayoitoa ili kuwa toleo maalum. Itakuwa na upana wa dhiraa elfu ishirini na tano, nao urefu wake kuanzia mashariki hadi magharibi utakuwa sawa na sehemu moja ya kabila; mahali patakatifu patakuwa katikati ya eneo hilo.
9 “Hiyo sehemu maalum mtakayotoa kwa Mwenyezi Mungu itakuwa na urefu wa dhiraa elfu ishirini na tano, na upana wa dhiraa elfu kumi.
10 Hii itakuwa ni sehemu takatifu kwa ajili ya makuhani. Itakuwa na urefu wa dhiraa elfu ishirini na tano upande wa kaskazini, upana wa dhiraa elfu kumi upande wa magharibi, dhiraa elfu kumi upande wa mashariki, na urefu wa dhiraa elfu ishirini na tano upande wa kusini. Katikati yake patakuwa mahali patakatifu pa Mwenyezi Mungu.
11 Hii itakuwa kwa ajili ya makuhani waliowekwa wakfu, Wasadoki, waliokuwa waaminifu katika kunitumikia, nao hawakupotoka kama Walawi walivyofanya wakati Waisraeli walipopotoka.
12 Itakuwa toleo maalum kwao kutoka sehemu takatifu ya nchi, yaani sehemu takatifu sana, inayopakana na nchi ya Walawi.
13 “Kando ya nchi ya makuhani, Walawi watakuwa na mgawo wa urefu wa dhiraa elfu ishirini na tano, na upana wa dhiraa elfu kumi. Urefu wake utakuwa jumla dhiraa elfu ishirini na tano, na upana wa dhiraa elfu kumi.
14 Hawataruhusiwa kuuza wala kuibadilisha hata mojawapo. Hii ndiyo sehemu nzuri ya nchi kuliko nyingine zote, hivyo haitakuwa mikononi mwa watu wengine, kwa sababu ni takatifu kwa Mwenyezi Mungu.
15 “Eneo linalobaki lenye upana wa dhiraa elfu tano, na urefu wa dhiraa elfu ishirini na tano litakuwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya mji, kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na maeneo ya malisho. Mji utakuwa katikati yake
16 nao utakuwa na vipimo hivi: upande wa kaskazini dhiraa elfu nne na mia tano, upande wa kusini dhiraa elfu nne na mia tano, upande wa mashariki dhiraa elfu nne na mia tano, na upande wa magharibi dhiraa elfu nne na mia tano.
17 Eneo la malisho kwa ajili ya mji litakuwa na eneo la dhiraa mia mbili na hamsini upande wa kaskazini, dhiraa mia mbili na hamsini upande wa kusini, dhiraa mia mbili na hamsini upande wa mashariki, na dhiraa mia mbili na hamsini upande wa magharibi.
18 Eneo linalobaki, linalopakana na sehemu takatifu likiwa na urefu sawa nalo, litakuwa dhiraa elfu kumi upande wa mashariki, na dhiraa elfu kumi upande wa magharibi. Mazao yake yatawapa watumishi wa mji chakula.
19 Watumishi wa mji wanaolima shamba hili watatoka katika makabila yote ya Israeli.
20 Eneo lote la hiyo sehemu litakuwa mraba, yaani dhiraa elfu ishirini na tano kila upande. Kama toleo maalum mtatenga sehemu takatifu, pamoja na milki ya mji.
21 “Eneo linalobaki pande mbili za eneo linalofanya sehemu takatifu na milki ya mji litakuwa mali ya mkuu anayetawala. Eneo hili litaenea upande wa mashariki, kuanzia kwenye dhiraa elfu ishirini na tano za sehemu takatifu hadi mpaka wa mashariki, na kuelekea upande wa magharibi, kuanzia kwenye dhiraa elfu ishirini na tano hadi mpaka wa magharibi. Maeneo haya mawili yanayoenda sambamba na urefu wa sehemu za makabila yatakuwa ya mkuu anayetawala, na sehemu ile takatifu pamoja na mahali patakatifu pa Hekalu itakuwa katikati yake.
22 Kwa hiyo milki ya Walawi na milki ya mji vitakuwa katikati ya eneo lile ambalo ni mali ya mkuu anayetawala. Eneo la mkuu anayetawala litakuwa kati ya mpaka wa Yuda na mpaka wa Benyamini.
23 “Kuhusu makabila yaliyobaki: “Benyamini atakuwa na sehemu moja; itakayoanzia upande wa mashariki hadi upande wa magharibi.
24 Simeoni atakuwa na sehemu moja; itakayopakana na nchi ya Benyamini kuanzia mashariki hadi magharibi.
25 Isakari atakuwa na sehemu moja; itakayopakana na nchi ya Simeoni kuanzia mashariki hadi magharibi.
26 Zabuloni atakuwa na sehemu moja; itakayopakana na nchi ya Isakari kuanzia mashariki hadi magharibi.
27 Gadi atakuwa na sehemu moja; itakayopakana na nchi ya Zabuloni kuanzia mashariki hadi magharibi.
28 Mpaka wa kusini wa Gadi utapita kusini kuanzia Tamari hadi maji ya Meriba-Kadeshi, kisha kupitia upande wa Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu.
29 “Hii ndiyo nchi mtakayogawanya kuwa urithi kwa makabila ya Israeli, nazo zitakuwa sehemu zao,” asema Bwana Mungu Mwenyezi.
30 “Haya yatakuwa ndiyo malango ya mji ya kutokea: “Kuanzia upande wa kaskazini, ambayo urefu wake ni dhiraa elfu nne na mia tano, utakuwa na malango matatu,
31 malango hayo ya mji yatapewa majina ya makabila ya Israeli. Malango hayo matatu ya upande wa kaskazini moja litakuwa lango la Reubeni, lango la Yuda na lango la Lawi.
32 Upande wa mashariki, wenye urefu wa dhiraa elfu nne na mia tano, utakuwa na malango matatu: lango la Yusufu, lango la Benyamini na lango la Dani.
33 Upande wa kusini, wenye urefu wa dhiraa elfu nne na mia tano, utakuwa na malango matatu: lango la Simeoni, lango la Isakari na lango la Zabuloni.
34 Upande wa magharibi, wenye urefu wa dhiraa elfu nne na mia tano, utakuwa na malango matatu: lango la Gadi, lango la Asheri na lango la Naftali.
35 “Urefu wote kuzunguka utakuwa dhiraa elfu kumi na nane. “Nalo jina la mji huo kuanzia wakati huo na kuendelea litakuwa: ‘Mwenyezi Mungu yupo hapa.’ ”
Перехресні посилання
126
- 1Ezk 47:15–17, Jos 19:40–47, 1Ki 12:28–29, Num 34:7–9, Mat 20:15–16, Jdg 18:26–29, Ezk 47:20, Num 1:5–15
- 2Jos 19:24–31, Gen 30:12–13
- 3Jos 19:32–39, Gen 30:7–8
- 4Jos 17:1–11, Jos 13:29–31, Gen 48:5, Gen 41:51, Gen 30:22–24, Gen 48:14–20
- 5Jos 17:8–10, Jos 17:14–18, Jos 16:1–10
- 6Jos 13:15–21, Gen 29:32, Gen 49:3–4
- 7Jos 15:1–63, Jos 19:9, Gen 29:35
- 8Isa 12:6, Ezk 45:1–6, Isa 33:20–22, Zec 2:11–12, Rev 21:22, Ezk 48:21, Ezk 48:35, 2Co 6:16
- 10Ezk 45:4, Ezk 44:28, Jos 21:1–45, Mat 10:10, Num 35:1–9, 1Co 9:13–14
- 11Ezk 40:46, Ezk 44:10, Mat 24:45–46, Ezk 43:19, 2Ti 4:7–8, Ezk 44:15–16, 1Pe 5:4, Rev 2:10
- 12Lev 27:21, Ezk 45:4
- 13Ezk 45:5, Ezk 45:3, Deu 12:19, Luk 10:7
- 14Lev 27:28, Lev 27:9–10, Lev 23:20, Mal 3:8–10, Lev 25:34, Lev 27:32–33, Exo 22:29, Ezk 48:12
- 15Ezk 45:6, Ezk 42:20, Ezk 44:23, Ezk 22:26, 1Ti 3:15
- 16Rev 21:16
- 18Ezr 2:43–58, Neh 7:46–62, Ezk 45:6, Jos 9:27
- 191Ki 4:7–23, Neh 11:1–36, Ezk 45:6
- 20Heb 12:17, Rev 21:16
- 21Ezk 48:22, Ezk 45:7–8, Hos 1:11, Ezk 48:10, Ezk 34:23–24, Ezk 37:24, Ezk 48:8
- 23Jos 18:21–28, Gen 35:16–19, Ezk 48:1–7
- 24Jos 19:1–9, Gen 29:33, Gen 49:5–7
- 25Jos 19:17–23, Gen 30:14–18
- 26Jos 19:10–16, Gen 30:19–20
- 27Jos 13:24–28, Gen 30:10–11
- 282Ch 20:2, Ezk 47:15, Ezk 47:19–20, Num 20:13, Num 34:5, Psa 106:32, Jos 13:3, Gen 14:7
- 29Num 34:2, Jos 13:1–21, Ezk 47:13–22, Num 34:13
- 30Ezk 48:16, Ezk 48:32–35, Rev 21:16
- 31Rev 21:12–13, Isa 26:1–2, Rev 21:25, Isa 60:11, Isa 54:12, Rev 21:21
- 35Rev 21:3, Zec 2:10, Rev 22:3, Isa 12:6, Jer 3:17, Jer 33:16, Isa 14:32, Jol 3:21