Hosea 13
1 Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka; alitukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali, naye akafa.
2 Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.”
3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani.
4 “Bali mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
5 Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
6 Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
7 Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
8 Kama dubu aliyenyang’anywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
9 “Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
10 Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
11 Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
12 Kosa la Efraimu limehifadhiwa, dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
13 Uchungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia, lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima; wakati utakapowadia hatatoka katika tumbo la mama yake.
14 “Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee Kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma,
15 hata ingawa Efraimu atastawi miongoni mwa ndugu zake. Upepo wa mashariki kutoka kwa Mwenyezi Mungu utakuja, ukivuma kutoka jangwani, chemchemi yake haitatoa maji na kisima chake kitakauka. Ghala lake litatekwa hazina zake zote.
16 Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao, kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini, wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”
Ngaahi fetuʻutaki veesi
122
- 1Hos 11:2, Gen 2:17, Luk 14:11, Num 27:16–23, Jos 3:7, Num 13:8, Jdg 12:1, Pro 18:12
- 2Isa 44:17–20, 1Ki 19:18, Isa 46:6, Jer 10:4, Hos 2:8, Hab 2:18–19, Rom 1:22–25, 2Ti 3:13
- 3Psa 68:2, Psa 1:4, Hos 6:4, Isa 17:13, Dan 2:35, Isa 41:15–16, Psa 83:12–17
- 4Isa 45:21–22, Hos 12:9, Exo 20:2–3, Isa 43:10–13, Isa 43:3, Act 4:12, Isa 44:6–8, Psa 81:9–10
- 5Deu 32:10, Deu 8:15, Deu 2:7, Psa 142:3, Gal 4:9, Nam 1:7, Exo 2:25, Psa 63:1
- 6Deu 32:13–15, Deu 8:12–14, Deu 6:10–12, Psa 10:4, Neh 9:35, Deu 32:18, Neh 9:25–26, Jer 2:31–32
- 7Jer 5:6, Hos 5:14, Lam 3:10, Isa 42:13, Amo 3:8, Amo 1:2, Amo 3:4
- 82Sa 17:8, Isa 5:29, Isa 56:9, Jer 12:9, Amo 9:1–3, Pro 17:12, Psa 80:13, Psa 50:22
- 9Jer 2:17, Jer 2:19, Deu 33:26, Psa 121:1–2, Pro 6:32, Isa 3:11, Hos 14:1, Jer 5:25
- 10Hos 8:4, 1Sa 8:5–6, Hos 10:3, Zec 14:9, Isa 43:15, 1Ki 12:20, Jer 8:19, Jer 2:28
- 111Sa 10:19, 1Sa 16:1, Pro 28:2, 1Ki 14:7–16, 1Sa 31:1–7, 1Sa 8:7–9, 2Ki 17:1–4, 1Sa 15:22–23
- 12Job 14:17, Deu 32:34–35, Rom 2:5, Job 21:19
- 13Isa 37:3, Isa 26:17, Isa 13:8, 2Ki 19:3, Psa 48:6, Mic 4:9–10, 1Th 5:3, Jer 49:24
- 14Isa 25:8, 1Co 15:52–57, Rev 21:4, Isa 26:19, Jas 1:17, Psa 49:15, 1Co 15:21–22, Psa 30:3
- 15Ezk 19:12, Ezk 17:10, Gen 41:52, Gen 48:19, Jer 4:11, Gen 49:22, Dan 11:8, Isa 14:21
- 162Ki 15:16, 2Ki 8:12, Psa 137:8–9, Isa 13:16, Amo 1:13, Nam 3:10, 2Ki 17:18, Amo 6:1–8
Topics in this chapter
38
Anger, Apostrophe, Baal, Backsliders, Chaff, Chimney, Cloud, Death, Dew, Drought, Ephraim, Forgetting God, God, Grave, Heart, Hell, House, Idolatry, Ingratitude, Israel, Israel, Prophecies Concerning, King, Leopard, Lion, Meteorology and Celestial Phenomena, Persia, Prisoners, Prosperity, Quotations and Allusions, Ransom, Resurrection, Saul, Silver, Sin, Smoke, War, Wicked (People), Wind