Hosea 10
1 Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
2 Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Mwenyezi Mungu atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
3 Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Mwenyezi Mungu. Lakini hata kama tungekuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
4 Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
5 Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
6 Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
7 Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya maji.
8 Mahali pa juu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
9 “Tangu siku za Gibea, umetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko ulibaki. Je, vita havikuwapata watenda maovu huko Gibea?
10 Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
11 Efraimu ni ndama jike aliyefundishwa ambaye hupenda kupura; hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
12 Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Mwenyezi Mungu, hadi atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
13 Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
14 mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, na ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
15 Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.
Ngaahi fetuʻutaki veesi
118
- 1Hos 8:11, Isa 5:1–7, Lev 26:1, Php 2:21, Hos 12:11, Rom 14:7–8, 1Ki 14:23, Jer 2:28
- 21Ki 18:21, Mic 5:13, Jas 4:4, Rev 3:15–16, Luk 16:13, Jas 1:8, Zep 1:5, Hos 8:5–6
- 3Hos 10:15, Hos 13:11, Hos 10:7, Hos 3:4, Jhn 19:15, Gen 49:10, Mic 4:9, Hos 11:5
- 4Hos 4:2, Amo 6:12, Amo 5:7, Deu 29:18, 2Ki 17:3–4, Ezk 17:13–19, Isa 59:13–15, Heb 12:15
- 5Hos 9:11, 2Ki 23:5, Hos 5:8, Hos 8:5–6, Hos 4:15, 1Sa 4:21–22, Hos 13:2, 2Ki 10:29
- 6Isa 30:3, Hos 5:13, Jer 7:24, Dan 11:8, Isa 44:9–11, Hos 4:7, Jer 2:36–37, Isa 45:16
- 7Hos 10:3, 2Ki 1:3, Jud 1:13, 2Ki 17:4, Hos 13:11, 2Ki 15:30, Hos 10:15, 1Ki 21:1
- 8Rev 6:16, Luk 23:30, Isa 2:19, 1Ki 12:28–30, Hos 9:6, Isa 32:13, Amo 8:14, 2Ch 34:5–7
- 9Hos 9:9, Jdg 20:5, Jdg 19:22–30, Gen 8:21, Gen 6:5, Mat 23:31–32, Jdg 20:13–14, Jdg 20:17–48
- 10Ezk 5:13, Hos 4:9, Jer 16:16, Zec 14:2–3, Deu 28:63, Ezk 23:9, Mic 4:10–13, Ezk 16:42
- 11Hos 4:16, Deu 25:4, Jer 50:11, Hos 11:4, Hos 3:1, Isa 28:24, Rom 16:18, Hos 9:1
- 12Jer 4:3–4, Jas 3:18, Isa 45:8, Pro 11:18, Isa 55:6, Hos 6:3, Jer 29:12–14, Isa 44:3
- 13Job 4:8, Gal 6:7–8, Pro 1:31, Pro 22:8, Hos 8:7, Pro 18:20–21, Psa 62:10, Hos 7:3
- 14Hos 13:16, Hab 1:10, 2Ki 18:9–10, Isa 22:1–4, 2Ki 18:33, Amo 9:5, Nam 3:10, Jer 48:41
- 15Hos 10:5, Hos 10:7, Rom 7:13, Amo 7:9–17, Hos 10:3, Isa 16:14
Topics in this chapter
44
Aven, Beth-Arbel, Beth-Aven, Calf, Character, Chastisement, Chemarim, Confidence, Covetousness, Cow, Desire, Despondency, Doubting, Gibeah, God, Grape, Heart, Heifer, Hemlock, Hoshea, Hypocrisy, Idolatry, Indecision, Israel, Prophecies Concerning, Jareb, Lukewarmness, Perjury, Pride, Quotations and Allusions, Reaping, Repentance, Righteousness, Rulers, Seed, Seekers, Shalman, Sin, Sower, Symbols and Similitudes, Thistle, Threshing, Unfaithfulness, War, Wicked (People)