Yuda 1
1 Yuda, mtumwa wa Isa Al-Masihi, na nduguye Yakobo.
2 Rehema, amani na upendo ziwe kwenu kwa wingi.
3 Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
4 Kwa kuwa kuna watu waliojipenyeza kwa siri kati yenu, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, waovu, wanaopotosha neema ya Mungu, na kuifanya kuwa ruhusa ya kutenda maovu, wakimkana Isa Al-Masihi, ambaye pekee ni Mtawala wetu mkuu na Bwana wetu.
5 Ingawa mmekwisha kujua haya yote, nataka niwakumbushe kuwa Mwenyezi Mungu, akiisha kuwaokoa watu wake kutoka nchi ya Misri, baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
6 Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu.
7 Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele.
8 Vivyo hivyo, hawa waotao ndoto huutia mwili unajisi, hukataa kuwa chini ya mamlaka na kunena mabaya juu ya wenye mamlaka.
9 Lakini hata malaika mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi kuhusu mwili wa Musa, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Mwenyezi Mungu na akukemee!”
10 Lakini watu hawa hunena mabaya dhidi ya mambo wasiyoyafahamu. Na katika mambo yale wanayoyafahamu kwa hisia kama wanyama wasio na akili, hayo ndiyo hasa yatakayowaangamiza.
11 Ole wao! Kwa kuwa wanaifuata njia ya Kaini, wamekimbilia faida katika kosa la Balaamu na kuangamia katika uasi wa Kora.
12 Watu hawa ni dosari katika karamu zenu za upendo, wakila pamoja nanyi bila hofu, wakijilisha wenyewe tu. Wao ni mawingu yasiyokuwa na maji, yakichukuliwa na upepo, miti isiyo na matunda wakati wa mapukutiko, ambayo hunyauka, iliyokufa mara mbili na kung’olewa kabisa.
13 Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele.
14 Idrisi, mtu wa saba kuanzia Adamu, alitoa unabii kuhusu watu hawa, akisema: “Tazama, Mwenyezi Mungu anakuja pamoja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake,
15 ili kumhukumu kila mmoja na kuwapatiliza wote wasiomcha Mungu kwa matendo yao yote ya uasi waliyoyatenda, pamoja na maneno yote ya kuchukiza ambayo wenye dhambi wamesema dhidi yake.”
16 Watu hawa ni wenye kunung’unika na wenye kutafuta makosa; wao hufuata tamaa zao mbovu; hujisifu kwa maneno makuu, na kuwasifu mno watu wengine kwa faida yao wenyewe.
17 Lakini ninyi wapendwa, kumbukeni yale mitume wa Bwana wetu Isa Al-Masihi waliyotabiri awali.
18 Kwa kuwa waliwaambia, “Siku za mwisho kutakuwa na watu wenye kudhihaki, watakaofuata tamaa zao wenyewe za upotovu.”
19 Hawa ndio watu wanaowagawanya ninyi, wanaofuata tamaa zao za asili, wala hawana Roho wa Mungu.
20 Lakini ninyi wapendwa, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho wa Mungu.
21 Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia rehema ya Bwana wetu Isa Al-Masihi, inayowapeleka katika uzima wa milele.
22 Wahurumieni walio na mashaka;
23 okoeni wengine kwa kuwanyakua kutoka motoni; nao wengine wahurumieni mkiwa na hofu, mkichukia hata vazi lenye mawaa na kutiwa unajisi na mwili.
24 Kwake yeye awezaye kuwalinda ninyi msianguke na kuwaleta mbele za utukufu wake mkuu bila dosari na kwa furaha ipitayo kiasi:
25 kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Isa Al-Masihi Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen.
Mga kaugnay na talata
185
- 11Pe 1:5, 1Th 5:23, 1Pe 2:9, Rom 1:1, Jhn 17:15, Jhn 14:22, 2Ti 1:9, Heb 3:1
- 22Pe 1:2, 1Pe 1:2, Rev 1:4–6, Rom 1:7
- 31Ti 6:12, Php 1:27, Jud 1:20, Tit 1:4, 2Ti 1:13, Rev 12:11, 2Ti 4:7–8, Rev 2:10
- 42Pe 2:1–3, Gal 2:4, 2Pe 2:10, Tit 1:15–16, 1Pe 2:16, 1Jn 2:22, 2Pe 2:18–22, 1Pe 2:8
- 5Heb 3:16–4:2, Num 26:64–65, 1Co 10:1–12, Psa 106:26, Num 14:22–37, Deu 2:15–16
- 62Pe 2:4, Mat 25:41, Eph 6:12, Mat 8:29, 2Pe 2:9, Heb 10:27, Rev 20:10, Jhn 8:44
- 7Deu 29:23, Rom 1:26–27, 2Pe 2:6, Gen 19:24–26, Gen 18:20, Gen 13:13, 1Co 6:9, Luk 17:29
- 8Heb 13:17, 2Pe 2:10–12, Exo 22:28, 1Pe 2:17, 1Ti 1:10, 1Co 3:17, Ecc 10:20, Jud 1:9–10
- 9Zec 3:2, 2Pe 2:11, Deu 34:6, Dan 12:1, Rev 12:7, Dan 10:21, Dan 10:13, 1Th 4:16
- 102Pe 2:12, Rom 1:21–22
- 112Pe 2:15, 1Jn 3:12, Rev 2:14, Gen 4:3–14, Heb 11:4, Num 16:1–35, Num 26:9–10, Jos 24:9–11
- 122Pe 2:17–20, Mat 15:13, Ezk 34:8, Pro 25:14, Php 3:19, Eph 4:14, 1Co 11:20–22, 2Pe 2:13–14
- 132Pe 2:17, Php 3:19, Isa 57:20, Psa 65:7, Rev 14:10–11, Rev 20:10, 2Ti 3:13, Jer 5:22–23
- 14Deu 33:2, Psa 50:3–5, 2Th 1:7–8, Heb 11:5–6, 1Th 3:13, Mat 16:27, Mat 25:31, Mat 24:30–31
- 151Co 4:5, Ecc 11:9, Rev 22:12–15, Rom 14:10, Rom 2:16, Psa 9:7–8, Psa 50:1–6, 1Sa 2:3
- 162Pe 2:18, Php 2:14, 2Pe 2:10, 1Ti 6:5, 1Co 10:10, 2Pe 3:3, Jud 1:18, 1Pe 4:2
- 172Pe 3:2, 1Jn 4:6, Eph 4:11, Act 20:35, Mal 4:4, Eph 2:20
- 182Pe 3:3, 2Ti 4:3, 2Ti 3:1–5, 2Ti 3:13, 1Ti 4:1–2, 2Pe 2:1, Act 20:29, Psa 14:1–2
- 191Co 2:14, Pro 18:1, Rom 8:9, Jas 3:15, Jhn 3:5–6, Heb 10:25, Hos 9:10, Isa 65:5
- 20Eph 6:18, Rom 8:26–27, 1Co 14:15, Col 2:7, 1Th 5:11, 1Co 14:4–5, Rom 8:15, 1Co 14:26
- 211Jn 4:16, Lam 3:25–26, Heb 9:28, Jhn 15:9–10, 2Pe 3:12, 2Th 3:5, Rev 12:11, Jhn 14:21
- 22Jas 5:19–20, Gal 6:1, 1Jn 5:16–18, Jud 1:4–13, Heb 6:4–8, Ezk 34:17, Gal 4:20
- 231Ti 4:16, 1Co 15:33, Rev 3:4, 2Co 7:10–12, 2Th 3:14, Rom 11:14, Zec 3:2–5, Rev 3:18
- 242Ti 4:18, Eph 3:20, Col 1:22, Jhn 10:29–30, Heb 13:20–21, Eph 5:27, 2Co 4:14, Rom 16:25–27
- 251Ti 1:17, Rev 5:13–14, Jhn 5:44, 1Pe 5:10–11, Rev 4:9–11, Rom 11:36, Isa 12:2, Psa 147:5