Ayubu 38
1 Kisha Mwenyezi Mungu akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakishangilia kwa furaha?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika hapa, wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonesha mapambazuko mahali pake,
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakung’uta waovu waliomo?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya muhuri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Umewahi kuoneshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika maghala ya theluji, au kuona maghala ya mvua ya mawe,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Njia iendayo mahali miali ya radi inapotawanywa ni ipi, au njia iendayo mahali upepo wa mashariki unaposambazwa juu ya dunia?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya miali ya radi,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 wakati maji yanakuwa magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unaganda?
31 “Je, unaweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Unaweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Unaweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Unaweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 “Unaweza kuipaza sauti yako hadi mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Je, wewe hutuma miali ya radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 mavumbi yanapokuwa magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
ข้ออ้างอิงโยง
226
- 1Job 40:6, 1Ki 19:11, 2Ki 2:11, Job 37:1–2, Exo 19:16–19, Nam 1:3, 2Ki 2:1, Job 37:9
- 2Job 42:3, 1Ti 1:7, Job 35:16, Job 34:35, Job 27:11, Job 23:4–5, Job 12:3, Job 24:25
- 3Job 40:7, Jer 1:17, Exo 12:11, 1Pe 1:13, 1Ki 18:46, Job 23:3–7, Job 13:22, Job 31:35–37
- 4Psa 104:5, Heb 1:10, Pro 30:4, Heb 1:2, Gen 1:1, Psa 102:25, Pro 8:29–30, Pro 8:22
- 5Isa 40:12, Zec 2:1–2, Job 11:9, Psa 78:55, Psa 19:4, Isa 40:22, 2Co 10:16, Pro 8:27
- 6Job 26:7, Psa 104:5, Psa 93:1, Isa 28:16, 2Pe 3:5, Psa 118:22, Zec 12:1, Eph 2:20–21
- 7Rev 5:11, Job 1:6, Ezr 3:11–12, Rev 22:16, Job 2:1, Rev 2:28, Psa 104:4, Zec 4:7
- 8Gen 1:9, Pro 8:29, Jer 5:22, Psa 104:8–9, Psa 33:7, Job 38:10
- 9Gen 1:2
- 10Psa 104:9, Jer 5:22, Psa 33:7, Job 26:10, Gen 9:15, Gen 1:9–10
- 11Psa 89:9, Pro 8:29, Psa 65:6–7, Mrk 4:39–41, Luk 8:32–33, Psa 93:3–4, Job 2:6, Isa 27:8
- 12Psa 74:16, Gen 1:5, Psa 148:3–5, Job 8:9, Luk 1:78, 2Pe 1:19, Psa 136:7–8, Job 15:7
- 13Job 37:3, Psa 104:35, Exo 14:27, Psa 19:4–6, Job 24:13–17, Psa 104:21–22, Psa 139:9–12
- 14Psa 104:6, Psa 104:2
- 15Psa 10:15, Job 18:5, Psa 37:17, Pro 4:19, Job 5:14, Job 18:18, Exo 10:21–23, Ezk 30:22
- 16Pro 8:24, Job 26:5–6, Psa 77:19, Jer 51:36
- 17Psa 9:13, Psa 107:18, Job 3:5, Psa 23:4, Psa 107:14, Psa 107:10, Job 12:22, Mat 4:16
- 18Psa 89:11–12, Rev 20:9, Jer 31:37, Isa 40:28, Psa 74:17, Job 28:24
- 19Ezk 32:8, Psa 104:20, Job 38:12–13, Mat 27:45, Gen 1:3–4, Isa 45:7, Gen 1:14–18, Deu 4:19
- 20Gen 10:19, Gen 23:17, Job 26:10
- 21Job 15:7, Job 38:12, Job 38:4
- 22Job 37:6, Psa 135:7, Psa 33:7, Job 6:16
- 23Jos 10:11, Isa 30:30, Exo 9:18, Job 36:13, Ezk 13:11–13, Rev 16:21, Exo 9:24, Job 36:31
- 24Job 38:12–13, Mat 24:27, Jon 4:8
- 25Job 28:26, Psa 29:3–10, Job 37:3–6, Job 36:27–28
- 26Jer 14:22, Psa 107:35, Heb 6:7–8, Isa 43:19–20, Isa 35:1–2, Psa 104:10–14, Job 36:27, Psa 147:8–9
- 27Psa 107:35, Psa 104:14
- 28Jer 14:22, Psa 147:8, Jer 10:13, Pro 3:20, Job 38:8, Gen 27:39, Deu 33:13, Jol 2:23
- 29Psa 147:16–17, Job 37:10, Job 38:8, Job 6:16
- 30Job 37:10
- 31Amo 5:8, Job 9:9
- 32Job 38:31, 2Ki 23:5, Job 9:9
- 33Jer 31:35–36, Gen 8:22, Job 38:12–13, Gen 1:16, Psa 148:6, Jer 33:25, Psa 119:90–91
- 34Job 22:11, Zec 10:1, Jas 5:18, Job 36:27–28, 1Sa 12:18, Amo 5:8
- 35Job 37:3, Job 36:32, Exo 9:23–25, 1Sa 22:12, Num 11:1, Isa 6:8, Exo 9:29, Isa 65:1
- 36Job 32:8, Psa 51:6, Pro 2:6, Ecc 2:26, Jas 1:5, Job 9:4, Exo 31:3, Jas 1:17
- 37Psa 147:4, Gen 8:1, Gen 15:5, Gen 9:15
- 39Psa 104:21, Psa 34:10, Job 4:10–11, Psa 145:15–16
- 40Job 37:8, Num 23:24, Gen 49:9, Num 24:9
- 41Luk 12:24, Psa 147:9, Mat 6:26, Psa 104:27–28
Topics in this chapter
34
Angel (A Spirit), Animals, Arcturus, Astronomy, Birds, Blessing, Clay, Condescension of God, Continents, Cornerstone, Darkness, Death, Gates, God, Hail, House, Ice, Job, Lightning, Man, Mazzaroth, Meteorology and Celestial Phenomena, Orion, Pleiades, Praise, Readings, Select, Speaking, Stars, Swaddle, Symbols and Similitudes, Whirlwind, Wisdom, Words, Zodiac