3 Yohana 1
1 Mzee.
2 Mpendwa, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kama vile roho yako ifanikiwavyo.
3 Ilinifurahisha sana baadhi ya ndugu walipokuja na kutueleza kuhusu uaminifu wako katika kweli na jinsi unavyoendelea kuenenda katika hiyo kweli.
4 Sina furaha kubwa kuliko hii, ya kusikia kwamba watoto wangu wanaenenda katika kweli.
5 Rafiki mpendwa, wewe ni mwaminifu kwa yale unayowatendea ndugu, ingawa wao ni wageni kwako.
6 Wameshuhudia kuhusu upendo wako mbele ya jumuiya ya waumini. Utafanya vyema ukiwasafirisha kama inavyostahili kwa Mungu.
7 Ilikuwa ni kwa ajili ya hilo Jina waliondoka, bila kukubali kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasiomwamini Al-Masihi.
8 Kwa hiyo imetupasa sisi kuonesha ukarimu kwa watu kama hao ili tuweze kutenda kazi pamoja kwa ajili ya kweli.
9 Nililiandikia kundi la waumini, lakini Deotrefe, yeye apendaye kujifanya wa kwanza, hakubali mamlaka yetu.
10 Hivyo nikija, nitakumbuka matendo yake atendayo, akitusingizia kwa maneno ya hila. Wala hatosheki na hayo anayotusingizia, bali pia hukataa kuwakaribisha ndugu, na hata huwazuia wale walio tayari kufanya hivyo na kuwafukuza watoke miongoni mwa waumini.
11 Rafiki mpendwa, usiige lile lililo baya bali lile lililo jema. Yeyote atendaye mema anatoka kwa Mungu, bali atendaye mabaya hajamwona Mungu.
12 Kila mtu ameshuhudia mema kuhusu Demetrio, vivyo hivyo hata na hiyo kweli yenyewe. Sisi pia twashuhudia mema juu yake, nanyi mwajua kwamba ushuhuda wetu ni kweli.
13 Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kuandika kwa kalamu na wino.
14 Badala yake, nataraji kukuona upesi, nasi tutaongea pamoja ana kwa ana.
15 Amani iwe kwako. Rafiki zetu walio hapa wanakusalimu. Wasalimu hao rafiki zetu walio huko, kila mmoja kwa jina lake.
Marejeleo mtambuka
99
- 11Jn 3:18, Rom 16:23, 1Co 1:14, 2Jn 1:1–13, Act 19:29, Act 20:4
- 22Pe 1:3–9, 2Pe 3:18, Col 1:4–6, 1Pe 4:8, 1Th 2:13–14, Psa 20:1–5, 2Th 1:3, 1Th 1:3–10
- 32Jn 1:4, 2Jn 1:2, 1Th 3:6–9, Rom 1:8–9, 2Co 7:6–7, 3Jn 1:4, 1Th 2:19–20, Psa 119:11
- 4Gal 4:19, 2Ti 1:2, Pro 23:24, 1Ti 1:2, 2Ki 20:3, 1Ki 2:4, Gal 2:14, 1Ki 3:6
- 5Gal 6:10, Luk 16:10–12, Col 3:17, Luk 12:42, Mat 24:45, 2Co 4:1–3, 1Pe 4:10–11
- 61Th 2:12, Tit 3:13, Act 15:3, Phm 1:5–7, Col 1:10, Php 4:14, Rom 15:24, 2Co 1:16
- 72Co 4:5, Rev 2:3, 2Ki 5:15–16, Col 1:24, 1Co 9:18, 2Co 11:7–9, 2Co 12:13, Act 5:41
- 81Co 3:5–9, 1Co 16:10–11, 2Co 6:1, Php 4:3, 2Co 8:23, 1Th 3:2, 2Co 7:2–3, Col 4:11
- 9Tit 1:7–16, Luk 22:24–27, Luk 9:48, Mat 23:4–8, Mrk 9:34, Mat 10:40–42, Php 2:3–5, Rom 12:10
- 10Isa 66:5, Luk 6:22, 2Co 13:2, Pro 10:8, Pro 10:10, 2Co 10:1–11, 1Co 5:1–5, 3Jn 1:5
- 11Isa 1:16–17, Psa 37:27, Eph 5:1, 1Pe 3:11, Jhn 3:20, 1Pe 3:13, Psa 34:14, 1Jn 3:6–9
- 121Ti 3:7, Jhn 21:24, Act 22:12, Act 10:22, Jhn 19:35, 1Th 4:12
- 132Jn 1:12
- 141Pe 5:14, Rom 16:1–16, Gen 43:23, Eph 6:23, Gal 5:16, Dan 4:1
- 15Jhn 10:3