Nehemia 12
1 Wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
2 Amaria, Maluki, Hatushi,
3 Shekania, Rehumu, Meremothi,
4 Ido, Ginethoni, Abiya,
5 Miyamini, Moadia, Bilga,
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
7 Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya.
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
9 Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
10 Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
11 Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
12 Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
13 wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
14 wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yusufu;
15 wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
16 wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
17 wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miyamini na ya Maazia, Piltai;
18 wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
19 wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
20 wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
21 wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
22 Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario Mwajemi.
23 Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
24 Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
25 Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
26 Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
27 Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
28 Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
29 kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
30 Makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kulingana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
31 Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
32 Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
33 pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
34 Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
35 pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
36 pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
37 Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
38 Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru hadi kwenye Ukuta Mpana,
39 juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, hadi kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
40 Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
41 na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
42 na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
43 Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
44 Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
45 Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Sulemani mwanawe.
46 Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa na viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
47 Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Haruni.
Referencias cruzadas
162
- 1Neh 10:2–8, Neh 12:12–21, Ezr 2:1–2, Neh 12:10, Mat 1:12–13, Hag 1:12, Ezr 3:8, Hag 1:14
- 4Luk 1:5
- 61Ch 9:10, Neh 11:10
- 7Ezr 3:2, Hag 1:1, Zec 3:1, Neh 12:1, 1Ch 24:18
- 8Neh 11:17, Neh 12:24, Neh 11:22, Neh 7:48, 1Ch 9:33, Neh 10:9–13, Neh 9:4
- 9Psa 134:1–3, Neh 12:24
- 10Neh 13:7, Neh 12:26, 1Ch 6:3–15, Neh 13:4, Neh 13:28, Neh 3:1
- 121Ch 15:12, 1Ch 24:6–31, 1Ch 9:33–34, Neh 12:22
- 22Neh 12:10–13
- 231Ch 9:14–44
- 241Ch 25:1–26, Neh 11:17, Jos 14:6, 1Ch 23:1–32, Neh 12:8–9, Neh 9:4, 2Ch 8:14, Ezr 2:40
- 251Ch 26:15, 1Ch 26:12, 1Ch 23:32, Isa 21:8, Neh 12:8–9, 1Ch 9:14–17, Neh 11:17–19
- 26Neh 8:9, Ezr 7:11, Ezr 7:6
- 271Ch 15:16, 2Ch 5:13, 1Ch 15:28, 2Ch 29:30, Deu 20:5, 1Ch 15:4, 1Ch 15:12, Psa 98:4–6
- 281Ch 9:16, 1Ch 2:54, Neh 6:2
- 29Neh 11:31, 1Ch 6:60, Deu 11:30, Jos 10:43, Jos 21:17, Ezr 2:24, Jos 5:9
- 30Exo 19:10, Job 1:5, Ezr 6:21, 2Ch 29:5, 2Ch 29:34, Heb 5:1, Neh 13:30, Neh 13:22
- 31Neh 2:13, Neh 12:38, Neh 3:13–14, Neh 12:40, 2Ch 5:2, 1Ch 13:1, 1Ch 28:1
- 33Neh 10:2–7
- 35Jos 6:4, Num 10:2–10, Neh 11:17, 1Ch 25:2, 2Ch 5:12, 1Ch 26:10–11, 1Ch 6:39–43, 2Ch 13:12
- 36Neh 12:24, 2Ch 8:14, 1Ch 23:5, Amo 6:5, Ezr 7:1, Ezr 8:1
- 37Neh 2:14, Neh 3:26, Neh 8:16, Neh 8:1, Neh 8:3, 2Sa 5:7–9, Neh 3:15–16
- 38Neh 3:8, Neh 3:11, Neh 12:31
- 39Neh 3:1, Neh 3:6, Neh 3:3, Neh 8:16, Neh 3:25, 2Ki 14:13, Zep 1:10, Jhn 5:2
- 40Psa 42:4, Neh 12:31–32, Psa 134:1–3, Psa 47:6–9
- 42Psa 81:1, Psa 95:1, Isa 12:5–6, Psa 98:4–9, Psa 100:1–2, Neh 11:14
- 43Ezr 3:13, Psa 92:4, Psa 148:11–13, Jer 31:13, Mat 21:9, Psa 28:7, Jhn 16:22, 2Ch 29:35–36
- 44Neh 10:37–39, Neh 13:12–13, 2Ch 31:11–13, 1Ch 26:21–26, Num 3:10, Isa 40:31, 1Ch 23:28, 2Ch 5:11–12
- 451Ch 25:1–26, 1Ch 23:28, 2Ch 23:6
- 462Ch 29:30, Psa 83:1, Psa 73:1, 1Ch 25:1–31
- 47Neh 12:26, Neh 12:1, Neh 11:23, Neh 13:10–12, Mal 3:8–10, Gal 6:6, Num 18:21–29, Neh 12:12
Temas en este capítulo
112
Abia, Adna, Akkub, Amariah, Amok, Asaph, Azareel, Azmaveth, Bakbukiah, Benjamin, Beth-Azmaveth, Bilgah, Binnui, Children, Cymbal, Darius, David, Dedication, Eber, Elam, Eleazar (Eleazer), Eliakim, Eliashib, Elioenai, Ephraim, Ezer, Ezra, Geba, Gilalai, Ginnethon, Hananeel, Hanani, Hananiah, Harim, Harp, Hashabiah, Hattush, Helkai, Hilkiah, Hoshaiah, Iddo, Israel, Prophecies Concerning, Jedaiah, Jehohanan, Jehonathan, Jehozadak, Jerusalem, Jeshua, Jezrahiah, Johanan, Joiada, Joiakim, Joiarib, Jonathan, Joseph, Joy, Judah, Kadmiel, Kallai, Levites, Maadiah, Maai, Maaseiah, Malchiah, Malluch, Mattaniah, Mattenai, Meah, Melicu, Meraiah, Meraioth, Meremoth, Meshullam, Miamin, Michaiah, Milalai, Miniamin, Moadiah, Music, Nehemiah, Nethaneel, Night, Obadiah, Offerings, Piltai, Porters, Priest, Psaltery, Rehum, Sallai, Seraiah, Shammua, Shealtiel, Shebaniah, Shechaniah, Sheep Gate, Shemaiah, Sherebiah, Solomon, Stairs, Talmon, Thankfulness, Tithes, Tower, Treasure-Houses, Trumpet, Unni, Uzzi, Zaccur, Zechariah (Zecharias), Zerubbabel, Zichri