Ezra 1
1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ili kulitimiza neno la Mwenyezi Mungu lililosemwa na nabii Yeremia, Mwenyezi Mungu aliusukuma moyo wa Koreshi mfalme wa Uajemi kutangaza katika himaya yake yote kwa maandishi:
2 “Hili ndilo asemalo Koreshi mfalme wa Uajemi: “ ‘Mwenyezi Mungu, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote duniani, na ameniagiza kumjengea Hekalu huko Yerusalemu katika Yuda.
3 Yeyote kati ya watu wa Mungu miongoni mwenu, Mungu wake na awe pamoja naye, wacha apande kwenda Yerusalemu katika Yuda na kujenga Hekalu la Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, Mungu aliyeko Yerusalemu.
4 Nao wakazi wa popote manusura wanapoishi sasa, wawape manusura fedha na dhahabu, pamoja na vifaa na mifugo, na sadaka za hiari kwa ajili ya Hekalu la Mungu huko Yerusalemu.’ ”
5 Kisha viongozi wa jamaa ya Yuda na Benyamini na makuhani na Walawi kila mmoja ambaye moyo wake ulisukumwa na Mungu, akajiandaa kupanda ili kuijenga nyumba ya Mwenyezi Mungu huko Yerusalemu.
6 Majirani zao wote wakawasaidia vyombo vya fedha na dhahabu, pamoja na vifaa na mifugo, pia na zawadi za thamani, pamoja na sadaka zote za hiari.
7 Zaidi ya hayo, Mfalme Koreshi akavitoa vyombo vilivyokuwa mali ya Hekalu la Mwenyezi Mungu, ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua kutoka Yerusalemu na kuviweka katika hekalu la mungu wake.
8 Koreshi mfalme wa Uajemi akavitoa kwa mkono wa Mithredathi mtunza hazina, aliyevihesabu mbele ya Sheshbaza mkuu wa Yuda.
9 Hii ilikuwa orodha ya vifaa: masinia ya dhahabu yalikuwa thelathini; masinia ya fedha yalikuwa elfu moja; vyetezo vya fedha vilikuwa ishirini na tisa;
10 mabakuli ya dhahabu yalikuwa thelathini; mabakuli ya fedha yaliyofanana yalikuwa mia nne na kumi; vifaa vingine vilikuwa elfu moja.
11 Kwa jumla, kulikuwa na vyombo elfu tano na mia nne vya dhahabu na vya fedha. Sheshbaza akavileta hivi vyote wakati watu walipotoka uhamishoni Babeli kwenda Yerusalemu.
Referencias cruzadas
72
- 1Jer 29:10, 2Ch 36:22–23, Jer 25:12–14, Ezr 6:22, Ezr 7:27, Jer 33:7–13, Pro 21:1, Ezr 5:13–15
- 2Isa 45:12–13, Isa 44:26–45:1, Dan 5:23, Dan 5:19–21, Dan 2:21, 2Ch 2:12, Dan 2:37–38, Dan 2:28
- 3Dan 6:26, Jer 10:10, Isa 45:5, Jos 1:9, Mat 28:20, Act 10:36, Psa 83:18, Deu 32:31
- 41Ch 29:3, Ezr 2:68–70, 1Ch 29:17, 1Ch 29:9, Ezr 7:16–18, Act 24:17, Gal 6:2, Ecc 4:9–10
- 5Ezr 1:1, 2Ch 36:22, Php 2:13, Neh 2:12, 2Co 8:16, Jas 1:16–17, 3Jn 1:11, Pro 16:1
- 62Co 9:7, Ezr 1:4, Ezr 8:25–28, Ezr 7:15–16, Psa 110:3, Ezr 8:33
- 72Ch 36:7, Ezr 6:5, 2Ki 24:13, Ezr 5:14, 2Ch 36:10, Dan 5:2–3, Jer 27:21–22, 2Ki 25:13–16
- 8Ezr 5:14, Ezr 5:16, Hag 1:1, Hag 2:2–4, Hag 1:14, Zec 4:6–10, Ezr 1:11
- 91Ki 7:50, Num 7:13, 2Ch 4:11, 2Ch 4:21–22, Mat 14:8, Mat 10:29–31, 2Ch 4:8, Num 7:19–89
- 11Rom 9:23, Mat 1:11–12, 2Ti 2:19–21
Pasajes paralelos
1
- The Decree of Cyrus2Ch 36:22–23, Ezr 1:1–4