Kumbukumbu La Torati 15
1 Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.
2 Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Mwenyezi Mungu wa kufuta madeni umetangazwa.
3 Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako.
4 Hata hivyo, hapatakuwa na maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana,
5 ikiwa tutamtii Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo.
6 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.
7 Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini.
8 Bali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji.
9 Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Mwenyezi Mungu dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.
10 Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako.
11 Siku zote watakuwa watu maskini katika nchi. Kwa hiyo ninawaamuru mwe wakarimu kwa ndugu zenu walio maskini na wahitaji katika nchi yenu.
12 Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.
13 Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu.
14 Mpe kwa hiari kutoka kundi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka, na kutoka shinikizo lako la kukamulia zabibu. Mpe kama vile Mwenyezi Mungu, Mungu wako, alivyokubariki.
15 Kumbukeni kuwa ninyi mlikuwa watumwa huko Misri naye Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, aliwakomboa. Ndiyo sababu nimewapa agizo hili leo.
16 Lakini mtumishi wako akikuambia, “Sitaki kukuacha,” kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako naye anaridhika nawe,
17 ndipo utachukua chuma kidogo utoboe sikio lake hadi hicho chuma kiingie kwenye ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako wa maisha. Ufanye vivyo hivyo kwa mjakazi wako.
18 Usifikiri kuwa kuna ugumu kumwacha mtumishi wako huru, kwa sababu utumishi wake kwako kwa miaka hii sita umekuwa wa thamani mara mbili ya ujira wa mtumishi wa kuajiriwa. Naye Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atakubariki kwa kila kitu utakachofanya.
19 Wekeni wakfu kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa makundi yenu ya ng’ombe na ya mbuzi na kondoo. Maksai walio wazaliwa wa kwanza msiwafanyize kazi, wala msinyoe manyoya ya wazaliwa wa kwanza wa kondoo.
20 Kila mwaka ninyi na jamaa zenu mtapaswa kuwala mbele za Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, pale mahali atakapopachagua.
21 Kama mnyama ana dosari, akiwa ni kilema au kipofu au kama ana kilema kibaya, kamwe usimtoe dhabihu kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.
22 Itawapasa kumla ninyi wenyewe katika miji yenu. Wote walio najisi na waliotakasika mwaweza kula kama vile mnavyokula paa au kulungu.
23 Lakini kamwe msile damu; imwageni ardhini kama maji.
Cross-references
129
- 1Deu 31:10, Exo 23:10–11, Lev 25:2–4, Exo 21:2, Luk 4:18–19, Jer 36:8–18, Isa 61:1–3
- 2Jas 2:13, Luk 7:42, Luk 6:34–38, Neh 5:7–11, Mat 18:25–35, Isa 58:3, Mat 6:14–15, Amo 8:4–6
- 3Deu 23:20, 1Co 6:6–7, Mat 17:25–26, Exo 22:25, Jhn 8:35, Gal 6:10
- 4Isa 58:10–11, Pro 28:27, Pro 11:24–25, Deu 28:1–8, Deu 14:29, Deu 28:11, Pro 14:21
- 5Deu 28:1–15, Php 1:27, Isa 1:19–20, Deu 11:13–15, Jos 1:7, Psa 19:11, Lev 26:3–14, Deu 4:9
- 6Deu 28:12–13, Luk 6:35, 1Ki 4:21, Pro 22:7, Neh 9:27, Ezr 4:20, Psa 37:21, Psa 37:26
- 7Deu 15:9, 1Jn 3:16–17, Pro 21:13, Jas 2:15–16, Mat 18:30
- 8Mat 5:42, Luk 6:34
- 9Deu 24:15, Mat 20:15, Jas 5:9, Mrk 7:21–22, Jer 17:10, Exo 22:23, Mat 15:19, Pro 23:6
- 10Pro 22:9, Heb 13:16, Psa 41:1–2, Isa 58:10, Deu 14:29, 1Ti 6:18–19, Deu 24:19, Php 4:18–19
- 11Mrk 14:7, Mat 26:11, Jhn 12:8, Deu 15:8, Pro 22:2, 1Jn 3:16–18, Act 4:32–35, Luk 12:33
- 12Jer 34:14, Exo 21:2–6, Lev 25:39–41, Deu 15:1, Jhn 8:35–36
- 13Jer 22:13, Mal 3:5, Pro 3:27–28, Exo 3:21, Gen 31:42, Col 4:1, Lev 25:42–44
- 14Pro 10:22, Act 20:35, 1Co 16:2, Psa 68:10, Neh 8:10
- 15Deu 16:12, 1Jn 4:9–11, Eph 2:12, Deu 5:14–15, Isa 51:1, 1Jn 3:16, Eph 4:32–5:2, Mat 18:32–33
- 16Exo 21:5–6, Psa 40:8, Psa 40:6
- 17Lev 25:39–42, 1Sa 1:22
- 18Isa 16:14, Luk 17:7–8, Isa 21:16
- 19Exo 13:2, Exo 13:12, Num 18:15, Deu 12:17, Num 18:17, Deu 16:14, Lev 27:26, Num 3:13
- 20Deu 12:5–7, Deu 12:17, Deu 14:23
- 21Mal 1:7–8, Deu 17:1, Lev 22:19–25
- 22Deu 12:21–22, Deu 12:15–16
- 23Deu 12:16, Lev 7:26, Deu 12:23, 1Sa 14:32, Ezk 33:25
Topics in this chapter
26
Aliens, Alms, Awl, Beneficence, Blessing, Blindness, Blood, Creditor, Employee, Fear, Firstborn, Fraternity, God, Hebrew, Humility, Lameness, Lending, Liberality, Poor, Reward, Sabbatic Year, Sanitation, Servant, Strangers, Wine Press, Year