Marko 15
1 Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa Torati na Baraza la Wayahudi lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Isa, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
2 Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi?” Isa akajibu, “Wewe umesema.”
3 Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
4 Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
5 Lakini Isa hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
6 Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
7 Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
8 Umati ule wa watu wakamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
9 Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu mfalme wa Wayahudi?”
10 Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Isa mkononi mwake kwa ajili ya wivu.
11 Lakini viongozi wa makuhani wakachochea umati ule wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita mfalme wa Wayahudi?”
13 Wakapiga kelele, wakisema, “Msulubishe!”
14 Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
15 Pilato, akitaka kuridhisha umati ule wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Isa apigwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
16 Askari wakampeleka Isa hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 Wakamvalisha Isa joho la zambarau, wakasokota taji la miiba, wakamvika kichwani.
18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
19 Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
20 Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
21 Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Iskanda na Rufo, alikuwa anaingia mjini kutoka mashambani, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
22 Kisha wakampeleka Isa hadi mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
23 Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
24 Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
25 Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: Mfalme wa Wayahudi.
27 Pamoja naye walisulubiwa wanyang’anyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
28 Nalo andiko likatimizwa, lisemalo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.”]
29 Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
30 basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
31 Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa Torati wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
32 Basi huyu Al-Masihi, huyu mfalme wa Israeli, ashuke sasa msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
33 Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
34 Hapo saa tisa, Isa akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
35 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Ilya.”
36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Isa ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Ilya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
37 Kisha Isa akatoa sauti kuu, akakata roho.
38 Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
39 Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Isa aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 Palikuwa na wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwa Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
41 Hawa walifuatana na Isa na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwako wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye hadi Yerusalemu.
42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi (yaani siku moja kabla ya Sabato),
43 Yusufu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na alikuwa anautarajia ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Isa.
44 Pilato alikuwa akijiuliza kama Isa alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Isa alikuwa amekwisha kufa.
45 Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yusufu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
46 Hivyo Yusufu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
47 Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.
Перехресні посилання
254
- 1Mat 27:1–2, Jhn 18:28–38, Act 3:13, Luk 22:66, Luk 23:1–5, Psa 2:2, Act 4:25–28, Mat 5:22
- 2Mat 2:2, Mat 27:11–14, 1Ti 6:13, Mrk 15:18, Mrk 15:26, Mrk 15:9, Jhn 19:19–22, Mrk 15:12
- 3Isa 53:7, Mat 27:12, Luk 23:2–5, Jhn 19:12, Jhn 19:6–7, Mrk 15:5, Mrk 14:60–61, Jhn 18:29–31
- 4Jhn 19:10, Mat 26:62, Mat 27:13
- 5Isa 53:7, Zec 3:8, Psa 71:7, 1Co 4:9, Mat 27:14, Isa 8:18, Jhn 19:9
- 6Jhn 18:39–40, Act 25:9, Act 24:27, Mat 26:2, Mat 27:15–26, Mat 26:5, Luk 23:16–25, Jhn 19:16
- 7Luk 23:18–19, Luk 23:25, Mat 27:16
- 9Mat 27:17–21, Jhn 19:14–16, Jhn 18:39, Act 3:13–15, Jhn 19:4–5
- 10Pro 27:4, 1Sa 18:8–9, Tit 3:3, Mat 27:18, Gen 4:4–6, Gen 37:11, 1Jn 3:12, Ecc 4:4
- 11Act 3:14, Mat 27:20, Hos 5:1, Jhn 18:40
- 12Isa 9:6–7, Jer 23:5–6, Mat 21:5, Zec 9:9, Mrk 11:9–11, Luk 23:2, Pro 2:6–7, Mat 27:22–23
- 14Luk 23:41, Isa 53:9, Luk 23:21, Jhn 18:38, Luk 23:47, Mat 27:4, Mat 27:19, Isa 53:3
- 15Isa 50:6, Jhn 19:1, Mat 27:26, Mrk 10:34, Pro 29:25, Psa 129:3, Jhn 19:16, Psa 57:11
- 16Mat 27:27–31, Jhn 19:9, Mat 26:3, Jhn 18:28, Jhn 18:33, Act 10:1
- 17Mat 27:28–30, Jhn 19:2–5, Luk 23:11
- 18Mat 27:42–43, Gen 37:20, Luk 23:36–37, Mrk 15:29–32, Gen 37:10, Jhn 19:14–15, Mrk 15:2
- 19Mrk 14:65, Isa 53:3–5, Rom 14:10–11, Mrk 10:34, Job 30:8–12, Psa 35:15–17, Luk 23:11, Mrk 9:12
- 20Mat 27:31, Jhn 19:16
- 21Luk 23:26, Mat 27:32, Rom 16:13, Act 6:9, Act 13:1, Act 2:10, Luk 14:27, Act 11:20
- 22Mat 27:33–44, Jhn 19:17–27, Luk 23:27–38
- 23Mat 27:34, Jhn 19:28–30, Luk 23:36, Luk 22:18, Mat 26:19, Mrk 14:25
- 24Luk 23:34, Jhn 19:23–24, Mat 27:35–36, Isa 53:4–8, Psa 22:16–18, 1Pe 2:24, 2Co 5:21, Deu 21:23
- 25Jhn 19:14, Luk 23:44, Mat 27:45, Mrk 15:33, Act 2:15
- 26Mat 27:37, Jhn 19:18–22, Zec 9:9, Luk 23:37–38, Mat 2:2, Mrk 15:2, Isa 10:7, Pro 21:1
- 27Mat 27:38, Luk 23:32–33, Jhn 19:18
- 29Mrk 14:58, Psa 109:25, Jhn 2:18–22, Lam 2:15, Lam 1:12, Psa 22:12–14, Psa 69:19–20, Mat 27:39–40
- 31Jhn 12:23–24, Psa 22:16–17, Psa 2:1–4, Mat 27:41–43, 1Pe 3:17–18, Luk 23:35–37, Jhn 11:47–52
- 32Mat 27:44, Luk 23:39–43, Mat 1:17, Zep 3:15, 2Ti 2:18, Zec 9:9, Isa 44:6
- 33Mat 27:45, Amo 8:9–10, Luk 23:44–45, Mrk 15:25, Isa 50:3–4, Psa 105:28
- 34Psa 22:1, Mat 27:46, Heb 5:7, Psa 27:9, Isa 41:17, Psa 71:11, Dan 9:21, Psa 42:9
- 35Mat 27:47–49, Mrk 9:11–13, Mat 17:11–13
- 36Psa 69:21, Mrk 15:23, Luk 23:36, Jhn 19:28–30
- 37Jhn 19:30, Luk 23:46, Mat 27:50
- 38Heb 10:19–23, Luk 23:45, Mat 27:51–53, Heb 9:3–12, Lev 16:2–19, Exo 26:31–34, Heb 4:14–16, Heb 6:19
- 39Mat 27:54, Luk 23:47–48, Mat 27:43, Act 10:1, Mat 8:5–10, Act 27:1–3, Mrk 15:44–45, Act 27:43
- 40Mat 27:55–56, Luk 23:49, Luk 8:2–3, Mat 27:61, Mat 13:55, Mat 28:1, Mrk 16:9, Mrk 15:47–16:1
- 41Mat 27:55–56, Luk 8:2–3
- 42Luk 23:50–56, Jhn 19:31, Mat 27:57–62, Jhn 19:38–42
- 43Luk 2:38, Luk 2:25, Luk 23:51, Act 17:12, Mat 27:57, Jhn 19:38, Act 4:8–13, Php 1:14
- 44Jhn 19:31–37
- 45Mat 27:58, Jhn 19:38, Mrk 15:39
- 46Isa 53:9, Mat 27:59–60, Mrk 16:3–4, Isa 22:16, Jhn 11:38, Mat 28:2, Jhn 19:38–42, Luk 23:53
- 47Mrk 15:40, Mrk 16:1, Mat 27:61, Mat 28:1, Luk 23:55–24:2
Паралельні місця
4
- Jesus before PilateMat 27:11–26, Mrk 15:1–15, Luk 23:1–25, Jhn 18:28–40
- The CrucifixionMat 27:32–44, Mrk 15:21–32, Luk 23:26–43, Jhn 19:16–27
- The Death of JesusMat 27:45–56, Mrk 15:33–41, Luk 23:44–49, Jhn 19:28–30
- The Burial of JesusMat 27:57–61, Mrk 15:42–47, Luk 23:50–56, Jhn 19:38–42
Теми в цьому розділі
82
Afflictions and Adversities, Alexander, Arimathea, Barabbas, Calvary, Centurion, Citizens, Civil Service, Complicity, Counsellor, Courage, Court, Criminals, Cross, Crown, Cyrene, Darkness, Day, Death, Decision, Demagogism, Eloi, Embalming, Envy, Galilee, Golgotha, Government, Homicide, Indictments, Inscriptions, Insurrection, Irony, James, Jerusalem, Jesus, the Christ, Joseph, Joses, Judge, Lama Sabachthani, Linen, Lot, the, Malice, Mary, Mocking, Myrrh, Opinion, Public, Passover, Persecution, Pilate, Pontius, Pleading, Politics, Preparation Day, Presumption, Pretorium, Priest, Prisoners, Prophecy, Punishment, Quotations and Allusions, Railing, Reed, Rufus, Rulers, Sabbath, Salome, Scourging, Self-Defense, Simon, Soldiers, Sponge, Stones, Sun, Superscription (Inscription), Theft and Thieves, Thorn, Unbelief, Vail, Verdict, Vinegar, Waiting, Wine, Women