Ayubu 2
1 Siku nyingine wana wa Mungu walienda kujionesha mbele za Mwenyezi Mungu. Shetani naye akaja pamoja nao kujionesha mbele zake.
2 Mwenyezi Mungu akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Mwenyezi Mungu, “Natoka kuzunguka duniani, nikitembea huku na huko.”
3 Mwenyezi Mungu akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, mtu asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. Naye bado anadumisha uadilifu wake, ingawa ulinichochea dhidi yake, ili nimwangamize pasipo sababu.”
4 Shetani akamjibu Mwenyezi Mungu, “Ngozi kwa ngozi! Mwanadamu atatoa vyote alivyo navyo kwa ajili ya uhai wake.
5 Lakini nyoosha mkono wako na kuipiga nyama yake na mifupa yake, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
6 Mwenyezi Mungu akamwambia Shetani, “Vema sana; kwa hiyo, yeye yumo mikononi mwako, lakini lazima umwachie uhai wake.”
7 Basi Shetani akatoka mbele za Mwenyezi Mungu, naye akampiga Ayubu kwa majipu mabaya tangu nyayo za miguu yake hadi utosi wa kichwa.
8 Ndipo Ayubu akachukua kigae na kujikuna nacho, huku akiketi kwenye majivu.
9 Mke wake akamwambia, “Je, bado unashikamana na uadilifu wako? Mlaani Mungu nawe ukafe!”
10 Akamjibu, “Unazungumza kama mwanamke mpumbavu. Je, tupokee mema kutoka kwa Mungu, bali tusipokee mabaya?” Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi katika kusema kwake.
11 Basi rafiki watatu wa Ayubu, ndio Elifazi Mtemani, na Bildadi Mshuhi na Sofari Mnaamathi, waliposikia kuhusu taabu yote iliyompata Ayubu, wakajipanga kutoka nyumbani mwao, wakakutana ili kwenda kumtuliza katika taabu hiyo na kumfariji.
12 Walipomwona kwa mbali, ilikuwa vigumu kumtambua. Wakaanza kulia kwa sauti kubwa, wakayararua majoho yao na kujirushia mavumbi juu ya vichwa vyao.
13 Kisha wakaketi chini kwenye udongo pamoja na Ayubu kwa siku saba usiku na mchana. Hakuna yeyote aliyesema naye neno, kwa sababu waliona jinsi mateso yake yalivyokuwa makubwa.
Ngaahi fetuʻutaki veesi
94
- 1Job 1:6, Heb 1:14, Luk 1:19
- 21Pe 5:8, Job 1:7, Jhn 14:30, 2Co 4:4, Gen 16:8
- 3Job 1:8, Job 9:17, Jas 1:12, Job 27:5–6, 1Pe 1:7, Pro 16:17, Php 3:12, Jhn 9:3
- 4Php 3:8–10, Mat 6:25, Mat 16:26, Jer 41:8, Est 7:3–4, Act 27:18–19
- 5Job 1:11, Lev 24:15, Job 1:5, Job 19:20–21, Job 2:9, Isa 8:21, Psa 38:2–7, Psa 32:3–4
- 61Co 10:13, Luk 22:31–32, Rev 2:10, Job 1:12, Luk 8:29–33, Job 38:10–11, Psa 65:7, Rev 20:1–2
- 7Deu 28:35, Isa 1:6, Job 30:30, Deu 28:27, Job 7:5, Rev 16:11, Isa 3:17, 1Ki 22:22
- 8Job 42:6, Jon 3:6, Ezk 27:30, Mat 11:21, Psa 38:5, Luk 16:20–21, Job 19:14–17, Psa 38:7
- 9Job 2:3, Job 2:5, Mal 3:14, 2Ki 6:33, Job 21:14–15, Gen 3:6, Job 1:11, 1Ki 11:4
- 10Jas 1:12, Lam 3:38–41, Job 1:21–22, Rom 12:12, Jas 5:10–11, Heb 12:9–11, Mat 16:23, Jhn 18:11
- 11Rom 12:15, Job 42:11, Job 6:14, Jer 49:7, Pro 17:17, Gen 25:2, 1Co 12:26, Job 19:21
- 12Lam 2:10, Ezk 27:30, Neh 9:1, Jos 7:6, Job 1:20, Lam 4:7–8, Rut 1:19–21, Est 4:1
- 13Gen 50:10, Neh 1:4, Ezk 3:15, Isa 3:26, Gen 1:8, Gen 1:5, Psa 77:4, Job 4:2