Ezekieli 35
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Mlima Seiri, utabiri dhidi yake
3 na useme: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Mimi ni kinyume nawe, ee Mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa.
4 Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
5 “ ‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake,
6 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mungu Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hukuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia.
7 Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaoenda.
8 Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote.
9 Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
10 “ ‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata Mimi Mwenyezi Mungu nilikuwa huko,
11 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mungu Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu.
12 Ndipo utakapojua kuwa Mimi Mwenyezi Mungu nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.”
13 Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia.
14 Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Dunia yote inaposhangilia, nitakufanya ukiwa.
15 Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee Mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’ ”
Ngaahi fetuʻutaki veesi
101
- 12Pe 1:21, Ezk 34:1, Ezk 22:1, Ezk 21:1
- 2Gen 32:3, Ezk 25:8, Ezk 6:2, Isa 34:1–17, Ezk 21:2, Isa 50:7, Isa 63:1–6, Eph 6:19
- 3Jer 6:12, Jer 15:6, Ezk 6:14, Ezk 35:7, Jer 21:13, Ezk 25:13, Nam 3:5, Jer 51:25
- 4Ezk 35:9, Mal 1:3–4, Ezk 6:6–7, Ezk 35:12, Jol 3:19, Exo 9:14, Exo 14:4
- 5Psa 137:7, Oba 1:10–16, Amo 1:11, Ezk 21:25, Ezk 21:29, Ezk 25:12, Ezk 25:15, Gen 27:41–42
- 6Isa 63:2–6, Oba 1:15, Rev 18:24, Rev 18:6, Rev 16:5–7, Psa 109:16–17, Rev 19:2–3, Mat 7:2
- 7Jdg 5:6–7, Ezk 29:11, Ezk 35:3, 2Ch 15:5–6, Ezk 33:28, Ezk 35:9
- 8Ezk 31:12, Ezk 39:4–5, Ezk 32:4–5, Isa 34:2–7
- 9Ezk 25:13, Mal 1:3–4, Ezk 35:4, Ezk 6:7, Ezk 36:11, Zep 2:9, Ezk 7:4, Jer 49:17–18
- 10Ezk 36:5, Ezk 48:35, Psa 83:4–12, Psa 48:1–3, Ezk 36:2, Psa 132:13–14, Zep 3:15, Oba 1:13
- 11Psa 9:16, Mat 7:2, Psa 73:17–18, Psa 137:7, Amo 1:11, Jas 2:13, Ezk 25:14
- 12Ezk 36:2, Psa 83:12, Psa 94:9–10, Jer 50:7, Ezk 35:9, Ezk 6:7
- 13Dan 11:36, 1Sa 2:3, Ezk 35:12, Isa 36:20, Jer 29:23, Job 35:16, Isa 10:13–19, Rev 13:5–6
- 14Isa 65:13–15, Isa 14:7–8, Jer 51:48
- 15Isa 34:5–6, Ezk 35:3–4, Lam 4:21, Oba 1:12, Oba 1:15, Psa 137:7, Ezk 36:2–5, Ezk 39:6–7