The Lord's Prayer
Biblia Takatifu (Swahili)
Mat 6:9–13
- 9 “Hivi ndivyo mnavyopaswa kuomba: “ ‘Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe.
- 10 Ufalme wako uje. Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
- 11 Utupatie riziki yetu ya kila siku.
- 12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tulivyokwisha kuwasamehe wadeni wetu.
- 13 Usitutie majaribuni, bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu [kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amen].’
Luk 11:1–4
- 1 Siku moja, Isa alikuwa mahali fulani akiomba. Alipomaliza kuomba, mmoja wa wanafunzi wake akamwambia, “Bwana Isa, tufundishe kuomba, kama vile Yahya alivyowafundisha wanafunzi wake.”
- 2 Akawaambia, “Mnapoomba, semeni: “ ‘Baba yetu [uliye mbinguni], jina lako litukuzwe, ufalme wako uje. [ Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.]
- 3 Utupatie kila siku riziki yetu.
- 4 Utusamehe dhambi zetu, kwa kuwa na sisi huwasamehe wote wanaotukosea. Wala usitutie majaribuni [bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu].’ ”