MEGA.Bible ค้นหา
ไทย

The Lord's Prayer

Biblia Takatifu (Swahili)

Mat 6:9–13

  1. 9 “Hivi ndivyo mnavyopaswa kuomba: “ ‘Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe.
  2. 10 Ufalme wako uje. Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
  3. 11 Utupatie riziki yetu ya kila siku.
  4. 12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tulivyokwisha kuwasamehe wadeni wetu.
  5. 13 Usitutie majaribuni, bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu [kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amen].’

Luk 11:1–4

  1. 1 Siku moja, Isa alikuwa mahali fulani akiomba. Alipomaliza kuomba, mmoja wa wanafunzi wake akamwambia, “Bwana Isa, tufundishe kuomba, kama vile Yahya alivyowafundisha wanafunzi wake.”
  2. 2 Akawaambia, “Mnapoomba, semeni: “ ‘Baba yetu [uliye mbinguni], jina lako litukuzwe, ufalme wako uje. [ Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.]
  3. 3 Utupatie kila siku riziki yetu.
  4. 4 Utusamehe dhambi zetu, kwa kuwa na sisi huwasamehe wote wanaotukosea. Wala usitutie majaribuni [bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu].’ ”