MEGA.Bible ค้นหา
ไทย

The Greatest Commandment

Biblia Takatifu (Swahili)

Mat 22:34–40

  1. 34 Mafarisayo waliposikia kwamba Isa alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.
  2. 35 Mmoja wao, mtaalamu wa Torati, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,
  3. 36 “Mwalimu, ni amri ipi katika Torati iliyo kuu kuliko zote?”
  4. 37 Isa akamjibu, “ ‘Mpende Mwenyezi Mungu, Mungu wako, kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’
  5. 38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
  6. 39 Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’
  7. 40 Amri hizi mbili ndizo msingi wa Torati na Manabii.”

Mrk 12:28–34

  1. 28 Mwalimu mmoja wa sheria akaja, akawasikia wakijadiliana. Akiona kwamba Isa amewajibu vyema, naye akamuuliza, “Katika amri zote, ni ipi iliyo kuu?”
  2. 29 Isa akajibu, “Amri iliyo kuu ndiyo hii: ‘Sikia ee Israeli. Mwenyezi Mungu, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.
  3. 30 Mpende Mwenyezi Mungu, Mungu wako, kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.’
  4. 31 Ya pili ndiyo hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’ Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.”
  5. 32 Yule mwalimu wa Torati akamwambia Isa, “Mwalimu, umejibu vyema kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye.
  6. 33 Kumpenda Mungu kwa moyo wako wote, na kwa ufahamu wako wote, na kwa nguvu zako zote, na kumpenda jirani kama mtu anavyojipenda mwenyewe ni bora kuliko kutoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu zote.”
  7. 34 Isa alipoona kwamba amejibu kwa busara, akamwambia, “Wewe huko mbali na ufalme wa Mungu.” Tangu wakati huo, hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumuuliza maswali tena.