MEGA.Bible ค้นหา
ไทย

The Beatitudes

Biblia Takatifu (Swahili)

Mat 5:1–12

  1. 1 Basi Isa alipoona makundi ya watu, alipanda mlimani akaketi chini, nao wanafunzi wake wakamjia.
  2. 2 Ndipo akaanza kuwafundisha, akisema:
  3. 3 “Heri walio maskini wa roho, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
  4. 4 Heri wale wanaohuzunika, maana hao watafarijiwa.
  5. 5 Heri walio wapole, maana hao watairithi nchi.
  6. 6 Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watatoshelezwa.
  7. 7 Heri wenye huruma, maana hao watapata rehema.
  8. 8 Heri walio na moyo safi, maana hao watamwona Mungu.
  9. 9 Heri walio wapatanishi, maana hao wataitwa wana wa Mungu.
  10. 10 Heri wanaoteswa kwa sababu ya haki, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
  11. 11 “Heri ninyi watu watakapowashutumu, na kuwatesa na kunena mabaya ya aina zote dhidi yenu kwa uongo kwa ajili yangu.
  12. 12 Furahini na kushangilia kwa maana thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwa kabla yenu.

Luk 6:20–23

  1. 20 Akawatazama wanafunzi wake, akasema: “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa sababu ufalme wa Mungu ni wenu.
  2. 21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka.
  3. 22 Mmebarikiwa ninyi, watu watakapowachukia, watakapowatenga na kuwatukana na kulikataa jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
  4. 23 “Furahini na kurukaruka kwa shangwe, kwa sababu thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo baba zao walivyowatenda manabii.