Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akawaambia Wareubeni, Wagadi na Manase, “Leo tunajua kwamba Mwenyezi Mungu yuko pamoja nasi, kwa sababu hamkukosa uaminifu kwa Mwenyezi Mungu katika jambo hili. Sasa mmewaokoa Waisraeli kutoka kwa mkono wa Mwenyezi Mungu.”