sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi arusi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Mwenyezi Mungu, wakisema, “ ‘ “Mshukuruni Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, kwa maana Mwenyezi Mungu ni mwema; fadhili zake zadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama ilivyokuwa hapo awali,’ asema Mwenyezi Mungu.