Mtu hatamfundisha tena jirani yake, wala mtu kumfundisha ndugu yake, akisema, ‘Mjue Mwenyezi Mungu,’ kwa sababu wote watanijua mimi, kuanzia aliye mdogo hata aliye mkubwa kuliko wote,” asema Mwenyezi Mungu. “Nitasamehe uovu wao, wala sitazikumbuka dhambi zao tena.”