Kwa kuwa hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu, yeye aliyeumba mbingu, ndiye Mungu; yeye aliyeifanya dunia na kuiumba, yeye ndiye aliiwekea misingi imara, hakuiumba ili iwe tupu, bali aliiumba ikaliwe na viumbe vyake. Anasema: “Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, wala hakuna mwingine.