Enyi mbingu, imbeni kwa furaha, kwa maana Mwenyezi Mungu amefanya jambo hili. Ee vilindi vya dunia, piga kelele. Enyi milima, pazeni sauti kwa nyimbo, enyi misitu na miti yenu yote, kwa maana Mwenyezi Mungu amemkomboa Yakobo, ameuonesha utukufu wake katika Israeli.