Huyo nabii au mwota ndoto lazima auawe, kwa sababu amehubiri uasi dhidi ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ambaye aliwatoa kutoka nchi ya Misri na kuwakomboa kutoka nchi ya utumwa; amejaribu kuwageuza kutoka njia ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, aliwaagiza mfuate. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu.