Kisha kuhusu mahali Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atakapopachagua kuwa makao ya Jina lake, hapo ndipo inapowapasa kuleta kila kitu ninachowaamuru: sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo, pamoja na vitu vyote vyenye thamani ambavyo mmeweka nadhiri kumtolea Mwenyezi Mungu.