Watu walioorodheshwa majina walikuja nchi hiyo wakati wa Hezekia mfalme wa Yuda. Wasimeoni wakawashambulia Wahamu katika makao yao pamoja na Wameuni ambao walikuwa huko, nao wakawaangamiza kabisa, kama ilivyo dhahiri hadi leo. Kisha wakaishi huko kwa sababu kulikuwa na malisho mazuri kwa mifugo yao.