Habakuki 2
1 Nitasimama katika zamu yangu, na kujiweka juu ya maboma; nitatazama nione atakaloniambia, na jibu nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.
2 Kisha Mwenyezi Mungu akajibu: “Andika ufunuo huu, na ukaufanye wazi juu ya vibao, ili mpiga mbiu akimbie nao.
3 Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika; unazungumzia mambo ya mwisho, na kamwe hautakosea. Iwapo utakawia, wewe usubiri; kwa hakika utakuja na hautachelewa.
4 “Tazama, amejaa majivuno; anavyovitamani si vya unyofu: lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:
5 hakika mvinyo humsaliti; ni mwenye kiburi na hana amani. Kwa sababu ni mlafi kama Kuzimu, na kama kifo kamwe hatosheki; anajikusanyia mataifa yote na kuchukua watu wote mateka.
6 “Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema, “ ‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu! Ataendelea hivi kwa muda gani?’
7 Je, wadai wako hawatainuka ghafula? Je, hawataamka na kukufanya utetemeke? Kisha utakuwa mhanga kwao.
8 Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi, watu waliobaki watakuteka nyara wewe. Kwa kuwa umemwaga damu ya watu; umeharibu nchi na miji, na watu wote wanaoishi humo.
9 “Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu, awekaye kiota chake juu, ili kukimbia makucha ya uharibifu!
10 Umepanga njama ya maangamizi ya watu wengi, ukiaibisha nyumba yako mwenyewe, na kupotewa na maisha yako.
11 Mawe ya kuta yatapiga kelele, na mihimili ya kazi ya mbao itarudisha mwangwi wake.
12 “Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!
13 Je, Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni hakuonesha kwamba kazi ya wanadamu ni mafuta tu kwa ajili ya moto, na kwamba mataifa yanajichosha bure?
14 Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu wa Mwenyezi Mungu, kama maji yaifunikavyo bahari.
15 “Ole wake yeye awapaye majirani zake kileo, akikimimina kutoka kwa kiriba cha mvinyo hadi wamelewa, ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.
16 Utajazwa na aibu badala ya utukufu. Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue! Kikombe kutoka mkono wa kuume wa Mwenyezi Mungu kinakujia, na aibu itafunika utukufu wako.
17 Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika, na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha. Kwa sababu umemwaga damu ya mtu; umeharibu nchi na miji na kila mmoja aliye ndani yake.
18 “Sanamu ina thamani gani, kwani mwanadamu ndiye alichonga? Ama kinyago kinachofundisha uongo? Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe; hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.
19 Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’ Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’ Je, linaweza kuongoza? Limefunikwa kwa dhahabu na fedha; hakuna pumzi ndani yake.
20 Lakini Mwenyezi Mungu yuko katika Hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze mbele yake.”
Marejeleo mtambuka
159
- 1Isa 21:8, Isa 62:6, 2Sa 18:24, Psa 85:8, Psa 73:16–17, Psa 5:3, 2Co 13:3, Jer 12:1
- 2Isa 30:8, Rev 14:13, Rev 1:18–19, Deu 31:22, Rev 21:5–8, Dan 12:4, Isa 8:1, Deu 27:8
- 3Psa 27:14, Heb 10:36–37, Ezk 12:25, Lam 3:25–26, Psa 102:13, Psa 130:5–6, Dan 10:14, Jas 5:7–8
- 4Rom 1:17, Heb 10:38, Gal 3:11–12, Gal 2:16, Jhn 3:36, 1Jn 5:10–12, Luk 18:14, Dan 4:37
- 5Pro 27:20, Isa 5:11–12, Pro 20:1, Pro 31:4–5, Isa 21:5, 2Ki 14:10, Isa 2:11–12, Pro 23:29–33
- 6Job 20:15–29, Jer 50:13, Isa 14:4–19, Num 23:7, Jer 29:22, Mic 2:4, Hab 1:15, Isa 44:20
- 7Pro 29:1, Isa 45:1–3, Dan 5:25–31, Isa 48:14–15, Isa 13:1–5, Ecc 10:8, Isa 46:11, Isa 13:16–18
- 8Isa 33:1, Hab 2:17, Jer 27:7, Psa 137:8, Zec 14:12, Jer 50:33–34, Jer 51:8, Isa 47:6
- 9Jer 49:16, Jer 22:13–19, 1Ki 21:19–24, Zec 5:1–4, Psa 52:7, Act 1:17–25, Oba 1:4, 2Ki 5:20–27
- 10Nam 1:14, 2Ki 9:26, Hab 2:16, 2Ki 10:7, Jer 36:31, Mat 27:25, Pro 1:18, Jer 22:30
- 11Luk 19:40, Jos 24:27, Jas 5:3–4, Job 31:38–40, Gen 4:10, Heb 12:24, Rev 6:10
- 12Mic 3:10, Nam 3:1, Dan 4:27–31, Jos 6:26, Jer 22:13–17, Rev 17:6, Jhn 11:47–50, Ezk 24:9
- 13Jer 51:58, Isa 50:11, Pro 21:30, Isa 55:2, Job 5:13–14, Isa 41:5–8, Psa 39:6, Psa 127:1–2
- 14Isa 11:9, Psa 22:27, Psa 72:19, Isa 6:3, Psa 86:9, Zec 14:8–9, Rev 11:15, Psa 67:1–2
- 15Jer 51:7, Gen 9:22, Hos 7:5, Rev 17:6, Rev 17:2, Rev 18:3, 2Sa 13:26–28, Exo 32:25
- 16Isa 47:3, Nam 3:5–6, Jer 25:26–29, Jer 25:15, Isa 49:26, Jer 51:57, Php 3:19, Isa 28:7–8
- 17Hab 2:8, Zec 11:1, Psa 55:23, Rev 18:20–24, Pro 28:17, Jer 50:33–34, Psa 137:8, Jer 51:24
- 18Jer 10:8, Zec 10:2, Isa 44:9–10, 1Co 12:2, Jer 2:27–28, Isa 42:17, Isa 45:16, Psa 115:4–8
- 19Psa 135:17, Jer 10:4, 1Ki 18:26–29, Jer 10:9, Dan 3:7, Dan 3:18, Isa 46:6, Psa 97:7
- 20Zec 2:13, Zep 1:7, Psa 46:10, Psa 11:4, Isa 6:1, Jon 2:7, Psa 76:8–9, Mic 1:2
Mada katika sura hii
31
Ambition, Blood, Carving, Character, Church, Covetousness, Drunkenness, Faith, Glory, Hell, Homicide, Idol, Idolatry, Jesus, the Christ, Justification, Minister, Christian, Oppression, Pride, Prophecy, Quotations and Allusions, Rulers, Self-Righteousness, Sin, Table, Vision, Waiting, Watchfulness, Wine, Word of God, Worship, Zeal, Religious