Ezekieli 32
1 Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Mwenyezi Mungu likanijia, kusema:
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Farao mfalme wa Misri na umwambie: “ ‘Wewe ni kama simba miongoni mwa mataifa, wewe ni kama mnyama mkubwa baharini, unapiga maji kwa kishindo katika vijito vyako, unayavuruga maji kwa miguu yako, na kuchafua vijito.
3 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Nikiwa pamoja na wingi mkubwa wa watu nitautupa wavu wangu juu yako, nao watakukokota katika wavu wangu.
4 Nitakutupa nchi kavu na kukuvurumisha uwanjani. Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako na wanyama wote wa nchi watajishibisha nyama yako.
5 Nitatawanya nyama yako juu ya milima na kujaza mabonde kwa mabaki yako.
6 Nitailowanisha nchi kwa damu yako inayotiririka njia yote hadi milimani, nayo mabonde yatajazwa na nyama yako.
7 Nitakapokuzimisha, nitafunika mbingu na kuzitia nyota zake giza; nitalifunika jua kwa wingu, nao mwezi hautatoa nuru yake.
8 Mianga yote itoayo nuru angani nitaitia giza juu yako; nitaleta giza juu ya nchi yako, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
9 Nitaifadhaisha mioyo ya mataifa mengi nitakapokuangamiza miongoni mwa mataifa, nikikuleta uhamishoni miongoni mwa nchi ambazo hujapata kuzijua.
10 Nitayafanya mataifa mengi wakustaajabie, wafalme wao watatetemeka kwa hofu kwa ajili yako nitakapotikisa upanga wangu mbele yao. Siku ya anguko lako kila mmoja wao atatetemeka kila dakika kwa ajili ya maisha yake.
11 “ ‘Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja dhidi yako.
12 Nitayafanya makundi yako kuanguka kwa panga za mashujaa: taifa katili kuliko mataifa yote. Watakivunjavunja kiburi cha Misri, nayo makundi yake yote yatashindwa.
13 Nitaangamiza mifugo yake yote wanaojilisha kando ya maji mengi: hayatavurugwa tena kwa mguu wa mwanadamu wala kwato za mnyama hazitayachafua tena.
14 Kisha nitafanya maji yake yatulie na kufanya vijito vyake vitiririke kama mafuta, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
15 Nitakapoifanya Misri kuwa ukiwa, na kuiondolea nchi kila kitu kilichomo, nitakapowapiga wote wanaoishi humo, ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’
16 “Hili ndilo ombolezo watakalomwimbia. Binti za mataifa wataliimba, kwa kuwa Misri na makundi yake yote wataliimba, asema Bwana Mungu Mwenyezi.”
17 Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
18 “Mwanadamu, omboleza kwa ajili ya makundi ya Misri na uwatupe Kuzimu, yeye na binti za mataifa yenye nguvu, waende huko pamoja nao wanaoshuka shimoni.
19 Je, ninyi mmekubalika zaidi ya wengine? Shukeni chini! Nanyi mkalazwe pamoja na hao wasiotahiriwa!
20 Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga. Upanga umefutwa; mwache aburutwe mbali pamoja na hao watu wake wote.
21 Kutoka Kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’
22 “Ashuru yuko huko pamoja na jeshi lake lote, amezungukwa na makaburi ya watu wake wote waliouawa, wale wote walioanguka kwa upanga.
23 Makaburi yao yako kwenye kina cha chini cha shimo na jeshi lake limelala kulizunguka kaburi lake. Wote waliokuwa wameeneza hofu kuu katika nchi ya walio hai wameuawa, wameanguka kwa upanga.
24 “Elamu yuko huko, pamoja na makundi yake yote wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote wameuawa, wameanguka kwa upanga. Wote waliokuwa wameeneza hofu katika nchi ya walio hai walishuka Kuzimu bila kutahiriwa. Wanaichukua aibu yao pamoja na wale wanaoshuka shimoni.
25 Kitanda kimetandikwa kwa ajili yake miongoni mwa waliouawa, pamoja na makundi yake yote wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote ni watu wasiotahiriwa, wameuawa kwa upanga. Kwa sababu vitisho vyao vilienea katika nchi ya walio hai, wameichukua aibu yao pamoja na wale wanaoshuka shimoni, nao wamewekwa miongoni mwa waliouawa.
26 “Mesheki na Tubali wako humo, pamoja na makundi yao wakiwa wameyazunguka makaburi yao. Wote hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga kwa sababu walieneza vitisho vyao katika nchi ya walio hai.
27 Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai.
28 “Wewe pia, ee Farao, utavunjwa nawe utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.
29 “Edomu yuko humo, wafalme wake wote na wakuu wake wote, ambao ijapokuwa wana nguvu, wamelazwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Wamelala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale wanaoshuka shimoni.
30 “Wakuu wote wa kaskazini na Wasidoni wote wako huko, wameshuka chini pamoja na waliouawa kwa aibu ijapokuwa kuna vitisho vilivyosababishwa na nguvu zao. Wamelala bila kutahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga na kuchukua aibu yao pamoja na wale wanaoshuka shimoni.
31 “Farao, yeye pamoja na jeshi lake lote, atakapowaona atafarijiwa kwa ajili ya makundi yake yote, wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
32 Ingawa nilimfanya Farao aeneze vitisho vyake katika nchi ya walio hai, Farao pamoja na makundi yake yote watalazwa miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mungu Mwenyezi.”
Marejeleo mtambuka
201
- 1Ezk 30:20, Ezk 32:17, Ezk 1:2, Ezk 31:1, Ezk 29:17, Ezk 29:1, Ezk 33:21
- 2Ezk 29:3, Nam 2:11–13, Ezk 27:2, Ezk 28:12, Jer 4:7, Ezk 32:16, Ezk 19:1–6, Isa 27:1
- 3Ezk 12:13, Jer 16:16, Lam 1:13, Ecc 9:12, Hab 1:14–17, Hos 7:12, Ezk 17:20
- 4Isa 18:6, Ezk 31:12–13, Ezk 29:5, Isa 34:2–7, Psa 63:10, Ezk 39:4–5, 1Sa 17:44–46, Psa 83:9–10
- 5Ezk 31:12
- 6Isa 34:3, Exo 7:17, Isa 34:7, Rev 14:20, Rev 16:6
- 7Mat 24:29, Jol 2:31, Jol 2:2, Isa 34:4, Isa 13:10, Ezk 30:3, Jol 3:15, Mrk 13:24
- 8Gen 1:14, Pro 20:20
- 9Rev 18:10–15, Ezk 29:12, Ezk 30:26, Jer 25:15–25, Ezk 30:23, Rev 11:18
- 10Ezk 27:35, Ezk 26:16, Exo 15:14–16, Deu 29:24, Deu 32:41, Ezk 30:9, Rev 18:10, Jer 51:9
- 11Jer 46:13, Jer 43:10, Ezk 30:4, Ezk 26:7, Jer 46:24–26, Ezk 30:22–25
- 12Ezk 28:7, Ezk 31:11, Ezk 29:19, Isa 25:2–3, Hab 1:6–7, Deu 28:49–50, Ezk 30:11
- 13Ezk 29:11, Ezk 29:8, Ezk 34:18, Ezk 30:12, Ezk 32:2
- 15Ezk 6:7, Exo 7:5, Exo 14:18, Exo 14:4, Ezk 29:12, Psa 9:16, Ezk 29:19–20, Psa 83:17–18
- 16Ezk 26:17, Ezk 32:2, 2Ch 35:25, 2Sa 1:17, Jer 9:17, 2Sa 3:33–34
- 17Ezk 32:1, Ezk 1:2, Ezk 33:21, Ezk 31:1
- 18Ezk 32:2, Ezk 31:14, Jer 1:10, Ezk 32:16, Mic 1:8, Hos 6:5, Ezk 26:20, Isa 16:9
- 19Ezk 32:29–30, Ezk 31:18, Jer 9:25–26, Ezk 28:10, Ezk 32:24, Ezk 31:2, Ezk 32:21, 1Sa 17:26
- 20Psa 28:3, Ezk 32:23–26, Pro 24:11, Jer 22:19, Ezk 32:29–30, Ezk 29:8–12
- 21Isa 14:9–10, Ezk 32:27, Ezk 32:24–25, Ezk 32:19, Luk 16:23–24, Num 16:30–34, Psa 9:17, Pro 14:32
- 22Ezk 32:26, Ezk 32:29–30, Ezk 32:24, Isa 37:36–38, Isa 30:33, Nam 1:7–12, Nam 3:1–19, Ezk 31:3–18
- 23Ezk 26:20, Ezk 26:17, Psa 27:13, Ezk 32:24–27, Job 28:13, Psa 116:9, Psa 142:5, Isa 14:15–16
- 24Ezk 32:30, Ezk 16:54, Ezk 32:25, Ezk 26:20, Ezk 16:52, Ezk 32:18, Jer 49:34–39, Gen 10:22
- 25Psa 139:8, Ezk 32:19, Ezk 44:9, Act 7:51, Ezk 32:21, 2Sa 1:20, 1Ch 10:4, Ezk 44:7
- 26Ezk 27:13, Gen 10:2, Ezk 39:1, Ezk 38:2–3, Ezk 32:27, Ezk 32:23–24, Ezk 32:32, Gen 10:12
- 27Isa 14:18–19, Job 3:13–15, Psa 109:18, Job 20:11, Ezk 32:21, Psa 92:9, Jhn 8:24, Pro 14:32
- 28Dan 2:34–35
- 29Jer 49:7–22, Oba 1:1–9, Amo 1:11–12, Isa 34:1–17, Gen 25:30, Isa 63:1–6, Ezk 35:1–15, Gen 36:1–19
- 30Ezk 38:6, Ezk 39:2, Ezk 38:15, Ezk 28:21, Ezk 32:24–25, Jer 25:22, Jer 25:26
- 31Ezk 31:16, Ezk 14:22, Lam 2:13
- 32Ezk 32:27, Heb 10:31, Job 31:23, Zep 3:6–8, 2Co 5:11, Gen 35:5, Rev 6:15–17, Jer 25:15–38