Zaburi 129
1 Wamenitesa sana tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
2 wamenitesa sana tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
4 Lakini Mwenyezi Mungu ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
5 Wale wote wanaoichukia Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Mwenyezi Mungu iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Mwenyezi Mungu.”