Zaburi 121

1 Nayainua macho yangu natazama milima: msaada wangu utatoka wapi?

2 Msaada wangu hutoka kwa Mwenyezi Mungu, Muumba wa mbingu na dunia.

3 Hatauacha mguu wako uteleze, yeye akulindaye hatasinzia,

4 hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.

5 Mwenyezi Mungu anakulinda, Mwenyezi Mungu ni uvuli wako mkono wako wa kuume,

6 jua halitakudhuru mchana, wala mwezi wakati wa usiku.

7 Mwenyezi Mungu atakukinga na madhara yote, atayalinda maisha yako,

8 Mwenyezi Mungu atakulinda unapoingia na unapotoka, tangu sasa na hata milele.