Nehemia 6
1 Habari zilipofika kwa Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu, na adui zetu wengine kwamba nimejenga tena ukuta na hakuna nafasi iliyobakia ndani yake, ingawa hata wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango,
2 Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Njoo, tukutane katika mojawapo ya vijiji katika nchi tambarare ya Ono.” Lakini walikuwa wakikusudia kunidhuru.
3 Kwa hiyo niliwatuma wajumbe kwao na majibu haya: “Kazi ninayoifanya ni kubwa sana, siwezi kuja. Kwa nini niiache kazi isimame nije kwenu?”
4 Walinitumia ujumbe huo huo mara nne, na kila mara nikawapa jibu lile lile.
5 Basi, mara ya tano, Sanbalati akamtuma msaidizi wake kwangu akiwa na ujumbe ule ule, naye alikuwa amechukua mkononi mwake barua isiyofungwa,
6 iliyokuwa imeandikwa: “Habari imeenezwa miongoni mwa mataifa, naye Geshemu anasema kwamba ni kweli, kuwa wewe na Wayahudi mnapanga njama ya kuasi, ndiyo sababu mnajenga ukuta. Zaidi ya hayo, kufuatana na taarifa hizi, karibuni utakuwa mfalme wao,
7 na hata umewateua manabii wafanye tangazo hili kukuhusu huko Yerusalemu: ‘Yuko mfalme katika Yuda!’ Sasa taarifa hii itarudishwa kwa mfalme. Basi njoo, tufanye shauri pamoja.”
8 Nilimpelekea jibu hili: “Hakuna jambo kama hilo unalosema linalofanyika. Unalitunga tu kwenye kichwa chako.”
9 Wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakifikiri hivi: “Mikono ya watu italegea kiasi kwamba hawataweza kufanya kazi, nayo haitakamilika.” Lakini niliomba, “Ee Mungu, sasa nitie mikono yangu nguvu.”
10 Siku moja nilienda nyumbani mwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, aliyekuwa amefungwa ndani ya nyumba yake. Akasema, “Tukutane katika nyumba ya Mungu, ndani ya Hekalu, na tufunge milango ya Hekalu, kwa sababu watu wanakuja kukuua. Naam, wanakuja usiku kukuua.”
11 Lakini nikasema, “Je, mtu kama mimi akimbie? Au mtu kama mimi aende Hekaluni kuokoa maisha yake? Sitaenda!”
12 Nilitambua kwamba Mungu hakumtuma, bali alitabiri dhidi yangu kwa sababu Tobia na Sanbalati walikuwa wamemwajiri.
13 Alikuwa ameajiriwa kunitisha ili kwa kufanya jambo hili nitende dhambi, kisha waweze kuniharibia jina langu na kuniaibisha.
14 Ee Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati kwa sababu ya yale waliyotenda. Pia kumbuka nabii mke Noadia na manabii wengine ambao wamekuwa wakijaribu kunitisha.
15 Basi ukuta ukakamilika siku ya ishirini na tano mwezi wa Eluli; kazi ilichukua siku hamsini na mbili.
16 Adui zetu wote waliposikia kuhusu hili, mataifa yote yaliyotuzunguka yakaogopa na kupoteza ujasiri, kwa sababu yalitambua kuwa kazi hii imefanyika kwa msaada wa Mungu wetu.
17 Pia katika siku hizo wakuu wa Yuda walikuwa wakituma barua nyingi kwa Tobia, nayo majibu yaliyotoka kwa Tobia yaliendelea kuwajia.
18 Kwa kuwa watu wengi katika Yuda walikuwa wamemwapia Tobia, kwani alikuwa mkwewe Shekania mwana wa Ara, na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti Meshulamu mwana wa Berekia.
19 Zaidi ya hayo, walikuwa wakiniarifu jinsi Tobia alivyo mtu mwema, nao walimwambia kila kitu nilichosema. Naye Tobia alituma barua za kunitisha.
Referências cruzadas
136
- 1Neh 2:10, Neh 2:19, Neh 4:1, Neh 3:3, Neh 4:6–7, Neh 3:1, Neh 3:6, Dan 9:25
- 21Ch 8:12, Psa 37:12, Neh 11:35, Luk 20:19–21, 2Sa 20:9, 2Sa 3:27, Psa 37:32, Pro 26:24–26
- 3Jhn 9:4, Mat 10:16, 1Ti 4:15–16, Pro 14:15, Luk 14:30, Ecc 9:10
- 4Luk 18:5, 1Co 15:58, Gal 2:5, Jdg 16:10, Jdg 16:15–20, Jdg 16:6, Pro 14:15, Pro 7:21
- 52Co 11:13–15, 2Th 2:10, 2Ki 18:26–28, Eph 6:11, 2Co 2:11
- 6Neh 2:19, Ezr 4:12, 1Pe 3:16, Rom 3:8, Mat 5:11, Jhn 19:13, Ezr 4:15, Luk 23:2
- 7Pro 26:24–26, Neh 6:12–13, 1Ki 1:34, Act 23:15, 1Ki 1:7, 1Ki 1:25, 2Sa 15:10–12, 1Ki 1:18
- 8Psa 52:2, Job 13:4, Jhn 8:44, Mat 12:34, Isa 59:4, Dan 11:27, Act 25:10, Act 24:12–13
- 9Psa 138:3, Eph 3:16, 1Sa 30:6, Php 4:13, Eph 6:10, Heb 12:12, Neh 4:10–14, 1Pe 5:10
- 10Jer 36:5, Psa 37:12, Mat 7:15, Ezr 10:31, 2Ch 28:24, Ezk 3:24, Pro 11:9, Psa 12:2
- 11Psa 11:1–2, Pro 28:1, Act 21:13, Luk 13:31–33, Php 2:17, Psa 112:8, Act 20:24, Psa 112:6
- 12Ezk 13:22, Jer 23:16, 1Ti 3:3, Tit 1:7, Act 20:33, 1Co 2:15, Ezk 13:19, Jer 14:14
- 13Jer 20:10, 2Co 11:12, Pro 29:5, Jas 4:17, Neh 6:6, 2Ti 1:7, Mat 26:59, Mat 10:28
- 14Neh 13:29, 2Ti 4:14–15, Mat 24:24, Jer 14:15, Ezk 13:16–17, 1Jn 5:16, Jer 28:15, Isa 9:14–15
- 15Neh 4:1–2, Psa 1:3, Ezr 6:15, Dan 9:25
- 16Psa 126:2, Jos 5:1, Neh 4:7, Neh 4:1, Neh 2:10, Act 5:38, Num 23:23, Exo 14:25
- 17Neh 3:5, Mat 24:10–12, Mic 7:1–6, Neh 5:7, Neh 13:28
- 18Ezr 2:5, Neh 7:10, Neh 3:30, Neh 3:4
- 19Pro 28:4, Jhn 7:7, Neh 6:13, Jhn 15:19, Isa 37:10–14, 1Jn 4:5, Neh 6:9, Act 4:18–21
Temas neste capítulo
45
Accusation, False, Afflictions and Adversities, Arah, Armies, Berechiah, Blessing, Bribery, Character, Church, Courage, Craftiness, Deception, Decision, Delaiah, Diplomacy, Elul, Falsehood, Fellowship, Gashmu, Geshem, God, Influence, Israel, Prophecies Concerning, Jerusalem, Johanan, Letters, Liberality, Malice, Mehetabeel, Minister, Christian, Month, Nehemiah, Noadiah, Ono, Prophets, Prophetesses, Sanballat, Shechaniah, Shemaiah, Strategy, Talebearer, Temple, Tobiah, Treachery, Women