Nehemia 1
1 Maneno ya Nehemia mwana wa Hakalia: Katika mwezi wa Kislevu katika mwaka wa ishirini, wakati nilikuwa ngomeni katika jumba la kifalme la Shushani,
2 Hanani, mmoja wa ndugu zangu, alikuja kutoka Yuda akiwa na watu wengine, nami nikawauliza kuhusu mabaki ya Wayahudi wale walionusurika kwenda uhamishoni na pia kuhusu Yerusalemu.
3 Wakaniambia, “Wale walionusurika kwenda uhamishoni, wale ambao wamerudi kwenye lile jimbo, wako katika taabu kubwa na aibu. Ukuta wa Yerusalemu umebomoka, na malango yake yamechomwa moto.”
4 Niliposikia mambo haya, niliketi, nikalia. Kwa siku kadhaa niliomboleza na kufunga na kuomba mbele za Mungu wa mbinguni.
5 Kisha nikasema: “Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa mbinguni, mkuu na mwenye kuogofya, ambaye hulishika agano lake la upendo na wale wanaompenda na kutii amri zake,
6 tega masikio yako, na ufungue macho yako, ili usikie maombi ya mtumishi wako anayoomba mbele yako usiku na mchana kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli. Ninaungama dhambi zetu sisi Waisraeli, pamoja na zangu na za nyumba ya baba yangu, tulizotenda dhidi yako.
7 Tumetenda uovu sana mbele zako. Hatukutii amri, maagizo na sheria ulizompa Musa mtumishi wako.
8 “Kumbuka agizo ulilompa Musa mtumishi wako, ukisema, ‘Mkikosa uaminifu, nitawatawanya miongoni mwa mataifa,
9 lakini mkinirudia na kutii amri zangu, ndipo hata kama watu wenu walio uhamishoni katika miisho ya dunia, nitawakusanya kutoka huko na kuwaleta mahali nilipopachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina langu.’
10 “Hawa ni watumishi wako na watu wako, uliowakomboa kwa nguvu zako kuu na mkono wako wenye nguvu.
11 Ee Bwana, tega sikio lako na usikie maombi ya huyu mtumishi wako, na maombi ya watumishi wako wanaofurahia kuliheshimu Jina lako. Nipe leo, mimi mtumishi wako, mafanikio kwa kunipa kibali mbele ya mtu huyu.” Kwa maana nilikuwa mnyweshaji wa mfalme.
Referências cruzadas
87
- 1Neh 10:1, Zec 7:1, Est 1:2, Dan 8:2, Ezr 7:7, Ezr 10:9, Est 3:15, Neh 2:1
- 2Neh 7:2, Ezk 6:9, Psa 137:5–6, Ezr 9:8–9, Ezr 9:14, Jer 44:14, Psa 122:6–9, Ezk 7:16
- 3Neh 2:17, 2Ki 25:10, Neh 2:3, Neh 2:13, Ezr 5:8, Neh 9:36–37, Neh 7:6, Jer 44:8–12
- 4Dan 9:3, Psa 137:1, Ezr 10:1, Psa 102:13–14, Neh 2:4, Psa 69:9–10, Zep 3:18, Dan 2:18
- 5Exo 20:6, Dan 9:4–19, Deu 7:21, Deu 7:9, Neh 4:14, 1Ki 8:23, Heb 6:13–18, Neh 9:32
- 6Dan 9:20, Dan 9:4, Psa 34:15, Psa 106:6, Dan 9:17–18, 2Ch 29:6, 2Ch 6:40, Isa 6:5
- 7Dan 9:5–6, Dan 9:11, Dan 9:13, Psa 106:6, Hos 9:9, Zep 3:7, Psa 19:8–9, Lev 27:34
- 8Deu 28:64, Deu 4:25–27, Lev 26:33–46, 1Ki 9:6–7, Deu 32:26–28, Luk 1:72, Psa 119:49
- 9Jer 29:11–14, Deu 30:2–5, Deu 4:29–31, Jer 32:37, Lev 26:39–42, Ezr 6:12, Deu 12:5, Mat 24:31
- 10Deu 9:29, Dan 9:15–27, Exo 32:11, Deu 15:15, Exo 13:9, Psa 136:12, Exo 15:13, Psa 74:2
- 11Neh 1:6, Neh 2:8, Neh 2:1, Pro 21:1, Heb 13:18, Ezr 7:6, Psa 130:2, Psa 86:6