Zaburi 142
1 Namlilia Mwenyezi Mungu kwa sauti, napaza sauti yangu kwa Mwenyezi Mungu anihurumie.
2 Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
3 Roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita, watu wameniwekea mtego.
4 Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
5 Ee Mwenyezi Mungu, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
6 Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
7 Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.