Zaburi 150

1 Msifuni Mwenyezi Mungu. Msifuni Mungu katika patakatifu pake, msifuni katika mbingu zake kuu.

2 Msifuni kwa matendo yake makuu, msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3 Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,

4 msifuni kwa matari na kucheza, msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,

5 msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila chenye pumzi na kimsifu Mwenyezi Mungu. Msifuni Mwenyezi Mungu!