The Beatitudes
Biblia Takatifu (Swahili)
Mat 5:1–12
- 1 Basi Isa alipoona makundi ya watu, alipanda mlimani akaketi chini, nao wanafunzi wake wakamjia.
- 2 Ndipo akaanza kuwafundisha, akisema:
- 3 “Heri walio maskini wa roho, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
- 4 Heri wale wanaohuzunika, maana hao watafarijiwa.
- 5 Heri walio wapole, maana hao watairithi nchi.
- 6 Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watatoshelezwa.
- 7 Heri wenye huruma, maana hao watapata rehema.
- 8 Heri walio na moyo safi, maana hao watamwona Mungu.
- 9 Heri walio wapatanishi, maana hao wataitwa wana wa Mungu.
- 10 Heri wanaoteswa kwa sababu ya haki, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
- 11 “Heri ninyi watu watakapowashutumu, na kuwatesa na kunena mabaya ya aina zote dhidi yenu kwa uongo kwa ajili yangu.
- 12 Furahini na kushangilia kwa maana thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwa kabla yenu.
Luk 6:20–23
- 20 Akawatazama wanafunzi wake, akasema: “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa sababu ufalme wa Mungu ni wenu.
- 21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka.
- 22 Mmebarikiwa ninyi, watu watakapowachukia, watakapowatenga na kuwatukana na kulikataa jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
- 23 “Furahini na kurukaruka kwa shangwe, kwa sababu thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo baba zao walivyowatenda manabii.