MEGA.Bible Suchen
Deutsch

Josiah's Passover

Biblia Takatifu (Swahili)

2Ki 23:21–23

  1. 21 Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
  2. 22 Hapakuwahi kuwa na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za waamuzi walioamua Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
  3. 23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Mwenyezi Mungu huko Yerusalemu.

2Ch 35:1–19

  1. 1 Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Mwenyezi Mungu katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
  2. 2 Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Mwenyezi Mungu.
  3. 3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Mwenyezi Mungu, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Sulemani mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, na watu wake Israeli.
  4. 4 Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Sulemani.
  5. 5 “Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu.
  6. 6 Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Mwenyezi Mungu kwa mkono wa Musa.”
  7. 7 Ndipo Yosia akawapa watu wote waliokuwepo wana-mbuzi na kondoo wapatao elfu thelathini kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ng’ombe elfu kumi; wote kutoka kwa mali binafsi ya mfalme.
  8. 8 Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi elfu mbili na mia sita, na mafahali mia tatu.
  9. 9 Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi elfu tano, na mafahali mia tano, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
  10. 10 Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru.
  11. 11 Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi.
  12. 12 Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Mwenyezi Mungu kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Musa. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali.
  13. 13 Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi.
  14. 14 Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani wazao wa Haruni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona hadi usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Haruni.
  15. 15 Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.
  16. 16 Kwa hiyo wakati ule, huduma yote ya Mwenyezi Mungu ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, na kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Mwenyezi Mungu, kama alivyoamuru Mfalme Yosia.
  17. 17 Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba.
  18. 18 Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi, na watu wote wa Yuda na wa Israeli waliokuwa huko, pamoja na wakaaji wa Yerusalemu.
  19. 19 Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.