Zaburi 23

1 Mwenyezi Mungu ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

2 Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,

3 hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4 Hata nikipita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji.

5 Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika.

6 Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Mwenyezi Mungu milele.