Zaburi 61

1 Ee Mungu, sikia kilio changu, usikilize maombi yangu.

2 Kutoka miisho ya dunia ninakuita, ninakuita huku moyo wangu unadhoofika; uniongoze kwenye mwamba ulio juu kuniliko.

3 Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu, ngome imara dhidi ya adui.

4 Natamani kukaa kwenye hema lako milele, na kukimbilia chini ya uvuli wa mabawa yako.

5 Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu, umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.

6 Mwongezee mfalme siku za maisha yake, miaka yake kwa vizazi vingi.

7 Mtawaze mbele za Mungu milele; amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.

8 Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.