Zaburi 46

1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.

2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa, na milima ianguke kilindini cha bahari,

3 hata maji yake yakinguruma na kuumuka, na milima itetemeke kwa mawimbi yake.

4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.

5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.

6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, yeye hupaza sauti yake, dunia ikayeyuka.

7 Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

8 Njooni mkaone kazi za Mwenyezi Mungu jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.

9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.

10 “Tulieni, mjue kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”

11 Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.