Zaburi 122
1 Nilishangilia pamoja na wale walioniambia, “Twende nyumbani mwa Mwenyezi Mungu.”
2 Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama malangoni mwako.
3 Yerusalemu imejengwa vyema kama mji ulioshikamana pamoja.
4 Huko ndiko makabila hukwea, makabila ya Mwenyezi Mungu, kulisifu jina la Mwenyezi Mungu kulingana na maagizo waliopewa Israeli.
5 Huko viti vya hukumu hukaa, viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.
6 Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu: “Wote wanaokupenda na wawe salama.
7 Amani na iwe ndani ya kuta zako, na usalama ndani ya ngome zako.”
8 Kwa ajili ya ndugu na rafiki zangu, nitasema, “Amani iwe ndani yako.”
9 Kwa ajili ya nyumba ya Mwenyezi Mungu, Mungu wetu, nitatafuta mafanikio yako.