Ayubu 25

1 Ndipo Bildadi Mshuhi akajibu:

2 “Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu; yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.

3 Je, majeshi yake yaweza kuhesabika? Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?

4 Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu? Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?

5 Ikiwa hata mwezi sio mwangavu nazo nyota si safi machoni pake,

6 sembuse mtu ambaye ni funza: mwanadamu ambaye ni buu tu!”