1 Msifuni Mwenyezi Mungu, ninyi nyote watumishi wa Mwenyezi Mungu, ninyi mnaotumika usiku ndani ya nyumba ya Mwenyezi Mungu.
2 Inueni mikono yenu katika patakatifu na kumsifu Mwenyezi Mungu.
3 Naye Mwenyezi Mungu, Muumba wa mbingu na dunia, awabariki kutoka Sayuni.