Zaburi 120

1 Katika dhiki yangu namwita Mwenyezi Mungu, naye hunijibu.

2 Ee Mwenyezi Mungu, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.

3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?

4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.

5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya mahema ya Kedari!

6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.

7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.