Tatnai
Zawadi, liwali wa Kiajemi (kiebrania pehah, yaani, “satrap;” kwa siku hizi “pasha”) “ng’ambo ya mto”, yaani, wa nchi yote iliyo magharibi ya Frati. Cheo hiki cha Kiebrania pehah hupewa maliwali wa majimbo kwa jumla. Alipewa Nehemia (5:14) na Zerubabeli (Hag. 1:1). Nyakati nyingine hutafsiriwa “jemadari” (1 Fal. 20:24; Dan. 3:2, 3), na nyakati nyingine tena “naibu” (Est. 8:9; 9:3). Pamoja na wengine, Tatnai alipinga kujengwa upya kwa hekalu (Ezr. 5:6); lakini kwa amri ya Dario, aliwasaidia Wayahudi (6:1-13).