MEGA.Bible Tafuta
Kiswahili

Calling the First Disciples

Biblia Takatifu (Swahili)

Mat 4:18–22

  1. 18 Isa alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa walikuwa wavuvi.
  2. 19 Isa akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
  3. 20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
  4. 21 Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Isa akawaita.
  5. 22 Nao mara moja wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.

Mrk 1:16–20

  1. 16 Isa alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa walikuwa wavuvi.
  2. 17 Isa akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
  3. 18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
  4. 19 Alipoenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
  5. 20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Isa.