Calling the First Disciples
Biblia Takatifu (Swahili)
Mat 4:18–22
- 18 Isa alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa walikuwa wavuvi.
- 19 Isa akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
- 20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
- 21 Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Isa akawaita.
- 22 Nao mara moja wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
Mrk 1:16–20
- 16 Isa alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa walikuwa wavuvi.
- 17 Isa akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
- 18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
- 19 Alipoenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
- 20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Isa.